sábado, 6 de junio de 2015

TAFAKARI: SHEREHE YA MWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTO

SHEREHE YA MWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTU
7/6/2015
Somo I: Kut  24:3-8
Zab: 116: 12-13, 15-18
Somo II: Ebr  9: 11-15
Injili: Mk 14: 12-16, 22-26
Nukuu:
"Musa akaenda akawaambia watu maneno yote ya Bwana, na hukumu zake zote; watu wote wakajibu kwa sauti moja, wakasema, Maneno yote aliyoyanena Bwana tutayatenda,” Kut 24:3

Musa akaitwaa ile damu, akawanyunyizia watu, akasema, Hii ndiyo damu ya agano alilolifanya Bwana pamoja nanyi katika maneno haya yote,” Kut 24:8

Lakini Kristo akiisha kuja, aliye kuhani mkuu wa mambo mema yatakayokuwapo, kwa hema iliyo kubwa na kamilifu zaidi, isiyofanyika kwa mikono, maana yake, isiyo ya ulimwengu huu, wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele,” Ebr 9:11-12

Basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai?” Ebr 9:14

Na kwa sababu hii ni mjumbe wa agano jipya, ili, mauti ikiisha kufanyika kwa kukomboa makosa yaliyokuwa chini ya agano la kwanza, hao walioitwa waipokee ahadi ya urithi wa milele,” Ebr 9:15 

 “Twaeni; huu ndio mwili wangu,” Mk 14:22b
“Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi,” Mk 14:24

Amin, nawaambia ninyi, Sitakunywa tena kabisa uzao wa mzabibu, hata siku ile nitakapounywa mpya katika ufalme wa Mungu,” Mk 14:25

TAFAKARI: “Huu ndio mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu!”
Wapendwa wana wa Mungu, leo Mama Kanisa anaadhimisha sherehe ya Mwili na Damu Takatifu ya Bwana wetu Yesu Kristo. Mbili kati sikukuu kubwa za Bwana wakati wa kipindi cha kawaida cha Mwaka wa Kanisa ni: Sherehe ya Mwili na Damu Takatifu ya Bwana wetu yetu Kristo  na Sherehe ya Moyo Mtakatifu wa Yesu. Jumapili hii katika mzunguko wa kiliturujia wa mwaka “B” wa Kanisa, Mama Kanisa anatupatia simulizi hili kutoka Mwinjili Marko.
Mungu kwa nyakati mbalimbali alifanya maagano na watu wake kwa malengo mbalimbali yakilenga ushirika wake na viumbe vyake, katika safari nzima ya kuvikomboa, na hasa mwanadamu kutoka katika utumwa wa dhambi. Agano hili lilifanya kuaminiana na kutekeleza maagizo yake kwa pande zote mbili. "Musa akaenda akawaambia watu maneno yote ya Bwana, na hukumu zake zote; watu wote wakajibu kwa sauti moja, wakasema, Maneno yote aliyoyanena Bwana tutayatenda,” Kut 24:3. Mungu haikumpasa kujisainisha katika agano kwa sababu yeye mwenyewe ni UAMINIFU, na kwamwe katika Ukuu wake hawezi kwenye kinyume chake mwenyewe.
Maagano haya kama ishara ikiwa ni kielelezo kwa upande wa binadamu iliendana na uteketezaji wa viumbe vingi visivyo na doa. Damu ya viumbe hili  vilihesabika maka ndiyo muhuri na kusahilisha muungano huu wa kiagano. Musa akaitwaa ile damu, akawanyunyizia watu, akasema, Hii ndiyo damu ya agano alilolifanya Bwana pamoja nanyi katika maneno haya yote,” Kut 24:8. Hivi ni hatua za awali katika safari nzima ya mwokovu wetu. Je, kwa nini Mungu hakulifanya jambo hili mara moja tu na watu wake wakamwelewa? Bila shaka tendo na safari hii ya wokovu wa Mwanadamu umepita katika hatua mbalimbali kwa lengo la kumfanya mwanadamu huyu atambue uzuri na umaana wa thamani ya wokovu wake, na uwepo wa Mungu katika maisha yake.
Wapendwa wana wa Mungu, Yesu Kristo ndiye anayebadili kabisa mwelekeo na mtazamo wa sadaka hizi za kuteketezwa. Lakini Kristo akiisha kuja, aliye kuhani mkuu wa mambo mema yatakayokuwapo, kwa hema iliyo kubwa na kamilifu zaidi, isiyofanyika kwa mikono, maana yake, isiyo ya ulimwengu huu, wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele,” Ebr 9:11-12. Kristo ndiye ukamilifu wa sadaka zote zile zitolewazo. Sababu kubwa ni Mungu amependezwa na  Kristo, “huyu ni Mwanangu, Mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye.” Mt 17:5. Tendo hili la utambulisha wa Kristo kile alicho lilitanguliwa na tendo la kumwilishwa kwake. Huu ndio mpango wa Mungu wakati ulipotimia. Hivyo, Basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai?” Ebr 9:14. Ndugu yangu unayemwamini Kristo elewa umekombolewa kwa damu yenye gharama kubwa. Ukristo wako ni wathamani sana. Hakuna sababu ya kujiona mnyonge hata kidogo. Na kwa sababu hii ni mjumbe wa agano jipya, ili, mauti ikiisha kufanyika kwa kukomboa makosa yaliyokuwa chini ya agano la kwanza, hao walioitwa waipokee ahadi ya urithi wa milele,” Ebr 9:15 
Hivyo wapendwa wana wa Mungu, leo tunaposherehekea sherehe hii, na zaidi tunapozama katika simulizi hili la kusimikwa rasmi kwa sherehe hii “Kitaasisi,” tendo hili latupasa kugusa ndani kabisa ya mioyo yetu, na haizi kabisa moyo wa kuhani. Ni kuhani wa Daraja Takatifu  ambaye hulifanya jambo hili na kuwa halisi  katika nafsi ya Yesu Kristo, zawadi ambayo hatuwezi kuielewa kwa mwono huo halisi Mbinguni. Ingawa ni ukweli usiotia shaka kwamba tunasheherekea ukuhani wetu siku ile ya upadrisho wetu na siku ya Alhamisi Kuu, je, haipaswi siku hii ya Sherehe ya Mwili na Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo, kuwa ya pekee kwa useja wetu wa Kiroho?
Injili ya leo tunakutana na maneno  mazito sana, “Twaeni; huu ndio mwili wangu,” Mk 14:22b. "wainjilisti nyingine huongeza," unaotolewa kwa ajili yenu.” Wapendwa wana wa Mungu, siyo tu  kwamba ni Mwili wa Yesu unaotolewa, bali miili yetu pia. Nina hakika nyote kwa asili mmegundua hatusemi "twaeni mle wote huu ni mwili wa Yesu uliotolewa kwa anjili yenu." Ingawa ni kweli mwili wa Yesu-ukweli  halisi wa uwepo wake, ambayo sisi tunasherehekea leo vizuri na kwa maandamano, lakini pia ni miili yetu iliyopondeka, miili ya dhambi iliyotolewa  sadaka kama kuhani / muathirika kwa ajili ya wokovu wa binadamu. Padre kujikatalia mke na watoto, si kwa sababu wao ni wabaya (mke na watoto), bali kwa sababu ni jambo jema sana kwa uwepo wao  la kutufanya sisi "Matowashi ajili ya Ufalme wa Mbinguni." Mt 19:12c
Ndugu yangu uzuri wa useja halisi kwa ajili ya Ufalme wa mbinguni kama sehemu ya ufundishaji wa teología/tauhidi ya Mwili, Baba Mtakatifu Yohane wa Pili  ananukuu Injili ya Mtakatifu Mathayo 19:21 na anafafanua juu ya zawadi ya useja ya kuhani kwa kutoka kwa Mungu na kutoka kwa Kuhani kwa ajili ya Kanisa. Anaeleza kwamba sisi-Makuhani tu uhuru tujongea uzuri wa ndoa kidunia na mahusiano ya kimapenzi kama ishara ya hali ile ambayo wanaume na wanawake  “wasivyoolewa au kujitoa katika ndoa.” Sisi "Tunapita juu-“Passover"- Sakramenti Takatifu ya ndoa kwa kutarajia/kuakisi " harusi ya Mwanakondoo." Sisi waseja ni ndoa ya kweli - ndoa ya ushirika wa Kristo na Kanisa lake. Tumepewa zawadi kubwa ya "upweke asili," ambayo kabla ya "umoja asili" katika shamba la Edeni, lakini, kwa wakati na mara nyingi,  maumivu ya upweke asili;  hujisikia upweke au mzigo. Mtazamo nyacha ni kwamba maumivu ni zawadi – mioyo yetu inahitaji kutakaswa na kuonekana hivyo na kuishi ukweli huo kwa furaha na uhuru.
Kama ilivyo mioyo mingi inayohitaji kutakaswa na wasiwasi,  wengi wanahitaji kusafishwa ya wasiwasi, shaka ya  kuona uwepo wa Yesu halisi katika Ekaristi Takatifu.  Huu ni wakati ambao hatutakiwi kurudi katika dhambi au kujionea huruma, lakini kwenye  maneno ya kuwekwa fumbo hili- “Twaeni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu.” Tunaweza kuliomba hili kwa Baba,  kwa  Kanisa, sisi wenyewe,  kwa  ukuhani, ambayo inahitaji utakaso wa  “kikafara/kutolewa sadaka” na maombezi  kwetu sisi makuhani, ikiwa ni pamoja na walei. Je, umeshajitoa sadaka, kufunga, kuomba na kupewa sadaka kwa ajili ya ndugu wanaojitahidi siku za hivi karibuni au wewe mwenyewe?
Kanisa ni Bibi harusi wetu,  mzuri na bila hitilafu kwa upande mmoja; dhambi, iliyoonekana na uliyopondeka kwa upande mwingine. Ni zawadi ya ajabu kwetu. Hivyo ndugu zangu, kwa Bibi harusi huyu imeachwa kuona michubuko yake, lakini hutaweza kuuona uzuri wake na heshima yake. Je, Bibi harusu huyu ni mwili wa Kristo au siyo?  Bibi harusi huyu dhahiri ni mwili wa Kristo. Anahitaji upendo wetu, uponyaji wetu, kumbatio letu, ulinzi wetu, heshima yetu, sadaka yetu na anahitaji ukuhani wetu na kitolewacho sadaka. Kanisa halihitaji mara kwa mara kulalamika na kusengenya. Kanisa linahitaji unyenyekevu wetu na umaskini wetu kama Kristo alivyojitoa mwenyewe kwa ajili yake.
Kwa upande wetu kama ndugu katika kanisa tunapoadhimisha Mbingu ile ni kweli, na Yesu amefufuka, na useja wetu ni ishara  huo. Jinsi  tunavyoadhimisha sadaka Takatifu ya Misa lazima kutafakari utashi wetu wa  umoja huu wa (upendo) kiuchumba kati ya Kristo na Kanisa lake. Sakramenti lazima iadhimishwe kwa upendo mkubwa na heshima, na si kwa haraka-“kwa kulipualipua au  kiroboti roboti.” Kama mume ajitoavyo  sadaka  kwa mke wake bila kujibakiza, mkewe haipaswi kuharakisha au kuchukulia jambo hili kwa wepesi tu. Lipi lililo la muhimu zaidi kwetu –Masakaramenti ya Mama Kanisa Takatifu au wajibu wa kiutawala ambao lazima tuufanye? Useja ukiliishwi vizuri, unachukua mabadiliko ya Kimungu, siyo tu malezi ya binadamu. Ni lazima kuwa na uwezo wa kuishi jambo hili kwa uhuru na hivyo kuchukua uponyaji na ukombozi kutoka utumwa wetu wa dhambi. Uwezo wa jambo hili kama dawa,  Kristo ametupa kwa njia ya  sala/maombi na kufunga. Vikwazo kwa mabadiliko na kuishi maisha halisi ya useja ni: dhambi isiyosemwa/kuungamwa, majeraha yasiyoponywa na  makosa yasiyosamehewa tuyapokeayo kutoka kwa wengine na sisi wenyewe. Tunajiheshimisha; na kuona hakuna haja ya kuwa na huruma kwetu wenyewe na kujiweka wenyewe kila siku mbele ya uponyaji wa uwepo wa Bwana wetu wa Ekaristi. Tendo hili haliwezi kuleta mabadiliko ndani mwetu kwa sababu bado hatujajisalimisha sawasawa.
Mwili na Damu Takakatifu ya Yesu ni uwepo alisi na inapaswa kuadhimishwa hivyo, lakini pia, sisi makuhani, licha ya kuonekana katika hali ya kupondeka, tunayo  haja ya kusherehekea uzuri halisi wa ukuhani, kwa sababu ni sisi, na kwa kushuka kwake Roho Mtakatifu,  anayefanya uwepo  alisi wa  Yesu katika Ekaristi Tatakatifu -Huu ndio mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu!
Bibi Betina kila mara alipohudhuria Misa Takatifu hakuacha kukominika kwa kutumia mikono yake. Tendo hili kwake lilikuwa la kawaida sana na hakuwa na subirá ya kuangalia mikono yake baada ya kuula mwili wa Kristo. Ila alikuwa na furaha sana siku moja akikutana na Yesu huko Mbinguni.
Miaka ilienda na mwisho wa uhai wake hapa duniani ulifikia kikomo. Basi alibahatika kumwona Yesu, lakini mara hii kama Hakimu mwenye haki. Mbele ya kiti hiki cha Hukumu, Yesu alimwuliza swali, Je, ulishawahi kukutana nami hata mara moja katika maisha yako? “Nimekutana nawe kila siku ya adhimisho la Misa Takatifu katika maumbo ya mkate na divai,” Bibi Betina alijibu kwa furaha.
Kwa masikitiko Yesu alimjibu, “Ni  kweli ulikutana nami katika maumbo hayo, ila hukuweza kukaa nami kwani ulinipokea na kunibwaga chini.” “Mbona sikuelewi Bwana wangu?” Bibi Betina alijibu kwa unyonge. “Ulinipokea katika mikono yako, na baada ya kula kile ulichokionekana kwa macho yako, hukuwa na muda wa kutazama mabakizo yangu. Ulijifuta mikono yako kwa mavazi ya nguo zako na mara nilidondoka chini na kukanyagwa na watu. Hivyo hukuwa na haja nami. Nibaki Kanisani.” Yesu alimjibu kwa utulivu. Hivyo huna makao yako huku. Nafasi zenu zipo upande ule wa pili kwenye barabara ile pana.

Hapa ndipo kwenye kilio na kusaga meno!


Tumsifu Yesu Kristo.

No hay comentarios:

Publicar un comentario