domingo, 14 de junio de 2015

TAFAKARI: JUMATATU WIKI YA 11 MWAKA-B

JUMATATU WIKI YA 11 YA MWAKA-B
15/6/2015
Somo: 2Kor 6:1-10
Zab: 97:1, 2-3ab, 3cd-4                                     
Injili: Mt 5:38-42
Nukuu:
Tusiwe kwazo la namna yo yote katika jambo lo lote, ili utumishi wetu usilaumiwe,” 2Kor 6:3
Kama wenye huzuni, bali siku zote tu wenye furaha; kama maskini, bali tukitajirisha wengi; kama wasio na kitu, bali tu wenye vitu vyote,” 2Kor 6:10

Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili,” Mt 5:39

Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo,” Mt 5:42 

TAFAKARI: “Tuongozane katika Utakatifu, na maisha yetu yawe ushuhuda wa kweli kama wafuasi wa Kristo.”

Wapendwa wana wa Mungu, licha ya kwamba kila mmoja wetu ameitwa kuishi mtindo wa wamaisha kadiri ya wito wake, “tuongozane  katika utakatifu, na maisha yetu yawe ushududa wa kweli kama wafuasi wa Kristo.” Kila mmoja kadiri ya wito wake unaoendana na mtindo wa maisha aliouchagua, anaitwa kuwa mtakatifu. Kwa sababu hii, mchango wangu kwa jamiii inayonizunguka nikuwafanya watu wajue thamani ya maisha yao, na waishi katika utimilifu huo wakitafuta zaidi ya kile walichokipata, utakatifu wao.

Hivyo, hatupaswi kuwa sababu ya mkwamo wa wowote juu ya  kumjiua, kumpenda, kumtumikia Mungu. Tusiwe sababu ya kuwakwaza watu katika imani yao. Tulipewa dhamana ya uongozi kadiri ya madaraja yetu, tumtambulishe Kristo kwa watu kama alivyo. Tusiwe kwazo la namna yo yote katika jambo lo lote, ili utumishi wetu usilaumiwe,” 2Kor 6:3. Wapo ambao kati yetu kila wanapokuwa badala ya kuimarisha imani wanakuwa chanzo cha mtafaruku wa Imani hiyo na kuwafanya waamini kuwa waasi wa Imani yao.

Kuishi maisha ya Kiimani kama yalivyo ni sadaka kubwa sana. Zipo nyakati ambazo utajaribiwa ili uonyeshe ukweli wa kila unachokiishi na unachokishuhudia kwa wengine. Hakuna sababu ya kujipamba kwa kile ambacho si chako na hukiishi. Mtazamo wetu katika uhasilia wa vitu ni huu: Kama wenye huzuni, bali siku zote tu wenye furaha; kama maskini, bali tukitajirisha wengi; kama wasio na kitu, bali tu wenye vitu vyote,” 2Kor 6:10. Matatizo katika maisha yetu hayapaswi kuwa ukuta wa kutufanya tusiweze kuona mbali. Matatizo ya hapa duniani yatuweke baribu na Mungu ili tuweze kutafakari vizuri neno lake.

Maisha yetu leo yametawaliwa na dhana ya ushindani na linganishi. Wapo kati yetu kila kukicha ni kutafuta zaidi ya kile alichokuwa nacho hata kama kinamtosha. Mtindo huu wa maisha hautoa taswira ya kushindwa au kuthamini  mchango wa wengine. Mwenye tabia hii  hujiamini kulikopindukia. Hivyo hapa inaitajika busara ya hali ya juu. Hivyo twapaswa kutoandamana na ya ulimwengu kama yanavyotutaka kila siku ya maisha yetu. Tuwe wepesi wa kusikiliza, na kusema pale tu pale inapotubidi kufanya hivyo.

Maadili ya Kikristo yanatuwasa mara zote kutokulipiza kisasa au kuishi katika visasi. Hivyo, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili,” Mt 5:39. Hapa tunafundishwa unyenyekevu katika kutenda. Ni katika utendaji huu kunatufanya kuwa karibu na kila mmoja wetu tutakaye kutana naye. Wote ni ndugu na jamaa zetu. Hivyo,  “Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo,” Kutokujali kama Mkristo ni kujivua vazi lako la Kikristo na kuvaa upangani au ushetani.

Tumsifu Yesu Kristo!


UTAKATIFU NDIYO CHEO CHETU, EE YESU  TUONGOZANE KATIKA UTUAKATIFU KILA SIKU. AMINA 

No hay comentarios:

Publicar un comentario