IJUMAA WIKI YA 3 YA MWAKA-I
Somo: Ebr 10:32-39
Zab: 37:3-4, 5-6, 23-24, 39-40
Injili: Mk 4:26-34
Nukuu:
“Basi msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kuu. Maana
mnahitaji saburi, ili kwamba mkiisha kuyafanya mapenzi ya Mungu mpate ile
ahadi,” Ebr 10:35-36.
“Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye
akisita-sita, roho yangu haina furaha naye,” Ebr 10:38
“Akasema, Ufalme wa Mungu, mfano wake ni kama mtu aliyemwaga
mbegu juu ya nchi,” Mk 4:26
“Ni kama
punje ya haradali, ambayo ipandwapo katika nchi, ingawa ni ndogo kuliko mbegu
zote zilizo katika nchi, lakini
ikiisha kupandwa hukua, ikawa kubwa kuliko miti yote ya mboga, ikafanya matawi
makubwa; hata ndege wa angani waweza kukaa chini ya uvuli wake,” Mk 4:31-32
TAFAKARI: “Madhara ya kuficha
na kutokukiri kosa ni kujiangamiza zaidi katika uovu.”
Wapendwa
wana wa Mungu, hakuna kati yetu asiyekuwa na mapungufu yake. Mapungufu yako yanathibitisha
ubinadamu wako. Kuyatambua mapungufu yako ni hatua muhimu sana kuelekea
ukamilifu ambao ndio wito wa kila mmoja wetu. “Basi
ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu,” Mt
5:48. Jambo la kushangaza ni kwamba kati yetu wapo ambo hawapendi na
hawayakubali mapungufu yao na kuchukua hatua kuelekea ukamilifu. Badala yake
huvaa vinyago ambavyo huwaharibu kabisa na kupoteza sura yao halisi. Wengi kati
yetu tunaisha maisha ya kuigiza ilhali kwa uhakika tunasutwa na dhamiri na
nafsi zetu.
Yesu leo anatupa aina mbili za mfano wa Ufalme wa Mungu. “Akasema, Ufalme wa Mungu, mfano wake ni kama mtu aliyemwaga
mbegu juu ya nchi,” Mk 4:26. Maana yake, anayezikuza mbegu hizo na kuwa kile
kilichokusudiwa na Mungu mwenyewe. “Basi msiutupe
ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kuu. Maana mnahitaji saburi, ili kwamba
mkiisha kuyafanya mapenzi ya Mungu mpate ile ahadi,” Ebr 10:35-36. Na
katika makuzi haya yaani maisha yako kila siku ni wakati wa wewe kuwa kile
Mungu alichokusudia uwe. “Sisi hatumo miongoni
mwao wasitao na kupotea, bali tumo miongoni mwa hao walio na imani ya kutuokoa
roho zetu,” Ebr 10:39. Hivyo ni wazi Mungu anapenda tuwe wanadamu kama
alivyotuumba kwa sura na mfano wake. Tunapojaribu kuwa kitu kingine ni chukizo
kwa Mungu na hapo tunakuwa wabaya kuliko hata shetani.
Mfano wa
pili wa Ufalme wa Mungu ni huu; “Ni kama punje ya haradali, ambayo ipandwapo
katika nchi, ingawa ni ndogo kuliko mbegu zote zilizo katika nchi, lakini ikiisha kupandwa hukua, ikawa
kubwa kuliko miti yote ya mboga, ikafanya matawi makubwa; hata ndege wa angani
waweza kukaa chini ya uvuli wake,” Mk 4:31-32. Hapa tunakumbushwa kwamba hakuna
kisicho na umaana mbele ya Mungu katika mwonekano wake, iwe ukubwa au udogo.
Hivyo hali yetu kama wafuasi wake Kristo pamoja na sintofahamu za maisha
tunazokabiliana nazo kila sikku, tunakumbushwa jambo hili la fadhila, yaani, “Maana mliwaonea huruma wale waliokuwa katika vifungo,
tena mkakubali kwa furaha kunyang'anywa mali zenu, mkijua kwamba nafsini mwenu
mna mali iliyo njema zaidi, idumuyo,” Ebr 10:34. Na mali hii njema ndani yetu
ni imani thabiti tuliyo nayo kwa Kristo Yesu. Na “mwenye haki wangu ataishi kwa
imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye,” Ebr 10:38
Ndugu yangu, vyote tuvionavyo
vinaudhihirisha Utukufu na Uzuri wa Mungu, na kwayo kwa kuwa kile kilicho
ufikia ukamilifu wake ambao ndio kusudio la kuumbwa kwake. Hivyo jipokee kama
ulivyo na yakamilishe yaliyo ndani yako kadiri ya mpango wa Mungu katika
ukamilifu wake.
Tumsifu
Yesu Kristo!
“Mikono yako ilinifanya ikanitengeneza, Unifahamishe
nikajifunze maagizo yako,” Zab 119
Tusali:-Ee Yesu Mwema, yakamilishe yote ndani yangu kwa sifa na
utukufu wako. Amina
No hay comentarios:
Publicar un comentario