DECEMBA 24, WIKI YA 4 YA MAJILIO
Somo: 2Sam 7:1-5, 8b-11, 14a, 16
Zab: 89:2-3, 4-5, 27, 29
Injili: Lk 1: 67-79
Nukuu:
“Je!
Wewe utanijengea nyumba, nikae ndani yake? Nalikutwaa
katika zizi la kondoo, katika kuwaandama kondoo, ili uwe mkuu juu ya watu
wangu, juu ya Israeli,” 2Sam 7:5b
“nami
nimekuwa pamoja nawe kila ulikokwenda, na kuwakatilia mbali adui zako wote
mbele yako; nami nitakufanyia jina kuu, kama jina la wakuu walioko duniani,”
2Sam 7:9
“Atukuzwe Bwana, Mungu
wa Israeli, Kwa kuwa amewajia watu wake, na kuwakomboa,” Lk 1:68
“Tuokolewe
na adui zetu Na mikononi mwao wote wanaotuchukia,” Lk 1.71
“Ya kwamba atatujalia
sisi, Tuokoke mikononi mwa adui zetu, Na kumwabudu pasipo hofu,” Lk 1:74
“Nawe, mtoto, utaitwa
nabii wake Aliye juu, Kwa maana utatangulia mbele za uso wa Bwana umtengenezee
njia zake; Uwajulishe watu wake wokovu, Katika kusamehewa dhambi
zao,” Lk 1:76
“Kuwaangaza wakaao
katika giza na uvuli wa mauti, Na kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani,”
Lk 1:79
TAFAKARI: “Kwa
kuwa amewajia watu wako, na kuwakomboa.”
Wapendwa
wana wa Mungu, kinachogusiwa katika somo letu la kwanza ni yale yaliyojiri
katika nyakati za mwisho za Mfalme Daudi. Ufalme wake katika miaka yake hiyo ya
mwisho ulikuwa imara na watu wake walifurahia amani ya kweli. Licha ya kwamba
Mfalme Daudi alimiliki jumba zuri la kifalme alikosa nyumba ya heshima kwa
ajili ya kuhifadhi sanduku la agano. Nabii Nathani anamkumbusha wajibu huo
muhimu wa kufanya Mfalme.
Ujumbe
wa Mungu kwa Mfalme Daudi ulisema hivi, “Je!
Wewe utanijengea nyumba, nikae ndani yake? Nalikutwaa
katika zizi la kondoo, katika kuwaandama kondoo, ili uwe mkuu juu ya watu
wangu, juu ya Israeli,” 2Sam 7:5b. Ujumbe huu ulimtaka Mfalme Daudi kwa ukarimu
wake uwe kigezo pia cha kuona ukarimu wa Mungu. Hivyo yampasa kufanya kitu
kuhusu Sanduku lile la Agano lihifadhiwe mahali pazuri zaidi. Yatupasa kuwa
wakarimu zaidi kwani kwa uwepo wetu duniani hapa ni ukarimu mkubwa sana wa
Mungu.
Hivyo
agano lililowekwa katika mlima sinai linawekwa katika uhalisia wake. Ujumbe huu
pia unahusisha yaliyosemwa na Nabii Isaya, 9:6, kwa kuzaliwa mtoto na mfalme wa
Amani, na uokoaji wake, Lk 1:32, 69, kwa kupewa kiti cha Baba yake Daudi na
kuwa pembe ya wokovu. Hivyo Masiha atakuwa mtoto wa Daudi, na ufalme wake
utakuwa ufalme wa milele. Undani wa habari hii tunakutana nao katika utenzi wa
Zakaria uliobeba Injili yetu ya leo.
Wapendwa
wana wa Mungu, “Zakaria akajazwa Roho Mtakatifu, na kutoa
unabii.” Maneno haya yanaonekana kutumika katika maana yake pana ya uhihisho
utamkwao katika hali ya kupongeza na sifa juu ya makuu mtu aliyotendewa na
yenye kustaajabia. Mfano wa hali hii tunakutana nayo (katika kitabu cha kwanza
cha Samueli 19:20; na waraka kwanza wa Mtume Paulo kwa Wakorintho 14: 24-25).
Utenzi au wimbo huu wa Zakaria
unaonekana kama taarifa iliyoandikwa, pengine, na Zakaria mwenyewe, kwa kusifu
mara maada ya kurudishiwa uwezo wake wa kuongea tena.
Maneno katika utenzi huu yawezekana ni
tafakari aliyokuwa nayo kipindi kizima cha yeye kutokuongea. Ni tafakari iliyozama
ndani kabisa katika matendo Makuu ya Mungu kwake na kwa Taifa zima la Israeli.
Utenzi wenyewe wa Zakaria ndio uliobeba Injili yetu ya leo. Ni vyema
tukatafakari kwa undani juu ya utenzi huu, Lk 1:67-80.
Zakaria alikuwa bubu alipoacha kuamini ujumbe
ule wa Malaika juu ya uwezo wa Mke wake kuzaa. Ububu wa Zakari ni matokeo ya
kutokuamini makuu ya Mungu. Midomo yake ikafunguka wakati alipoamini. Zakaria
ni wa mwisho kati ya Manabii wa Agano la Kale, ingawa Yohane yeye alikuja
kukaribisha Angano Jipya {Mathayo 11: 9 - Mathayo 11:11}. Kwa maana hiyo,
Zakaria alikuwa nabii wa mwisho wa mpango wa Agano la Kale, kabla ya kuja kwa
mtoto wake kwa kuhusisha Agano la Kale na Agano Jipya], aliyekuwa karibu sana
na kuja kwake Masiha. Wimbo wa Zakaria unachukua Mwangwi wa zamani zote, na
kuviyeyusha ndani ya mwanga mpya wa matumaini.
Utenzi au wimbo huu wa Zakaria tunaweza
kuugawa katika sehemu kuu tatu: sehemu ya kwanza ni {Luka 1:68 - Luke 1:75},
habari tukutanayo hapa ni kuhusu adhimisho la
kuja kwa Masihi, kwa namna ya pekee katika kuikomboa Israeli kutoka
maadui zake. Sehemu ya pili ni {Luka
1:76 Luka 1:77}, habari za sehemu hii zipo katika lugha ya picha zaidi juu ya
sintofahamu ya huyu ‘mtoto’ Yohane. Na sehemu ya tatu na ya mwisho, {Luke 1:78
- Luke 1:79}, inaturudisha katika wazo msingi kuhusu Masiha, lakini sasa
linagusa juu ya suala la kuja kwake kama Mwanga kwa wote wanaokaa katika giza.
Kama tunakumbuka kwamba miaka mia nne ya
sintofahamu juu ya Taifa hili la Israeli, kwa sehemu kubwa Waisraeli walikuwa
chini ya mateso na dola ya kigeni, ilikuwa imepita tangu mwisho wa
Manabii. Hivyo kwa wakati huo wote macho yao mchana na usiku
yalionekana kunyong'onyea kwa kumsubiri
Masiha aliyeahidiwa. Katika mazingira haya na ishara zilizokuwa zinaambatana na
tukio hili, ni wazi sasa tunaweza kuona yaliyokuwa yameujaza moyo wa Zakaria.
Ni wazi kwa ishara hizo saa imewadia, na kwamba mtoto hivi karibuni kuzaliwa
atatimiza ahadi ya Mungu na kukidhi matumaini yake yaliyoanza kutoweka.
Si ajabu kwamba maneno yake ya kwanza ni
mpasuko wa baraka za 'Mungu kwa wa
Israeli.' “Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, Kwa kuwa amewajia watu wake, na
kuwakomboa,” Lk 1:68. Haya ni matamshi yaliyo bora na ya hali ya juu ya furaha,
wakati mtu akielekea kukata tamaa na mara unatokea mwaka na kuondoa giza lote.
Ni shukrani kwa Mungu. Hapa tunaona ni kwa namna gani muda unakuwa mfupi wa
kusubiri, na hali ya kukosekana kwa uvumilivu ambayo iligubikwa kwa kusubiri!
Zakaria inazungumzia ukweli ambao ushakamilika!
Zakaria anajua fika kwamba Umwilisho
ushakamilia. Hii inajidhihirisha kwa maneno yake ya mkazo katika utenzi wake;
'amekuja kuwakomboa, amekwisha kukombolewa, alimfufua' ni Nabii, kuashiria
uhakio lijalo. Zakaria atakuwa anajua pia Famili ya Kifalme ya Maria kwa asili,
kwa namna anavyo sema juu ya 'mlango wa Daudi.' “Ametusimamishia pembe ya
wokovu Katika mlango wa Daudi, mtumishi wake,” Lk 1:69
'Pembe' ya wokovu ni
nembo iliyo chukuliwa kutoka wanyama, na ina maanisha nguvu. Maneno haya
yanakumbuka unabii kadhaa, na kama wajibu na utambulisho wa Masihi, vivuli na
ushindi mkuu, ni kwa ajili ya ukombozi kwa watu wake. Maono yaliyo mbele ya
Zakaria ni yale ya umshindi wa Mfalme Daudi uliotabiriwa kwa muda mrefu na
manabii, ambao utaiweka Israeli huru kutoka maadui na wakandamizaji wake wa
kigeni, ikiwa ni pamoja na dola ya
Kirumi. Hivyo ni Mungu mwenyewe ataye watembelea na kuwaokoa watu wake.
“Ya kwamba atatujalia sisi, Tuokoke mikononi mwa adui zetu, Na kumwabudu pasipo
hofu,” Lk 1:74.
Kuna aina mbili za kutembelewa katika hali
ya Kimungu, moja ikiwa kwa huruma na nyingine kwa hukumu. Wazo la wokovu
Kimasiha limeelezwa kwa upana na kuinuliwa vya kutosha katika sehemu hii ya
Injili, Lk 1:71-Lk 1:75. Neno 'ukombozi'
limeelezewa vizuri kama ilivyo kwa maelezo ya 'pembe ya wokovu.' Ukombozi
umebeba masuala mazito ambayo pia huonekana ni makusudi ya Mungu. Jambo hili
hujionyesha katika hali tatu zilizofungamana: kwanza, kwa kuonyesha huruma kwa
Mababa waolikufa kutokana na safari hii
katika historia ya wokovu. Hili ni wazo
kuu, na mwono utokao hapa kama pumziko lililotukuka na lenye heshima ya juu
kabisa. Tendo hili laonyesha wakishiriki katika furaha ya kuja kwake Masiha, na
pengine katika baraka ambazo Yeye, Masiha anazileta. Hali hii ni zaidi ya lugha
ya picha. Ni zaidi ya yale yanayoweza kufikirika.
Suala la pili ni kukumbukwa kwa ahadi zake
Mungu, au kwa maneno mengine, kutimizika kwa ahadi zake. Mwisho ni kwamba taifa
lililowekwa huru, lazima limtumikie Mungu. “Ya kwamba atatujalia sisi, Tuokoke
mikononi mwa adui zetu, Na kumwabudu pasipo hofu, Kwa utakatifu na kwa
haki Mbele zake siku zetu zote,” Lk 1:74-75. Ukombozi wa nje ulikuwa mbele ya
macho ya watu watauwa kama Zakaria ambao ushirika wao ulikuwa kama njia
mojawapo ya kufikia mwisho. Uhuru wa kisiasa ulikuwa lazima kwa utumishi wa
Mungu, na ulithaminiwa hasa kama kielelezo cha kufikia hazma hiyo. Katika
Utenzi huu, Zakaria unaibua mambo muhimu sana ambayo wana wa Israeli hawakuwa
huru kuyafanya ndani ya dola zile za kigeni. Hivyo, 'uhuru wa kuabudu Mungu,'
na Mungu kuabudiwa’ ni moja mtazamo wa Zakaria kuhusu nyakati za Kimasiha, Lk
1:74-75.
Ukitazama matumizi ya neno huduma ya
kikuhani, Kuhani Zakaria hajasahau kwamba kwa kadiri ya mwongozo na mtazama wa
awali, Waisraeli wote walikuwa Taifa la Makuhani. Kwa mtazamo huu, naye Zakaria
anamatazamio hayo yenye kuelekea ukamilisho wa jambo hili, na uwezekano wa
kubadilishwa kwa mpango wake katika ukuhani kwa wote. Kwa maana nyingine
Zakaria hajui kwa kina ukweli anaouimba. Mwisho wa kuja kwake Kristo, na wa
ukombozi ambayo Yeye anafanya kwa ajili yetu kutoka mikono ya adui zetu, ukweli
huu hauwezwi kusema vizuri zaidi ya maneno haya. ‘Tunakombolewa ili tupate kuwa
makuhani kwa Mungu na kwa Mungu.’
Huduma yetu ya kikuhani lazima itolewe
katika 'utakatifu na haki,' katika kuwekwa wakfu kwa Mungu na utekelezaji wa
majukumu yote. Hivyo haipaswi kuingiliwa au kuwa huduma ya mara chache, kama
Zakaria, ambayo alihudumu wiki mbili
katika mwaka. Hata hivyo utenzi huu wa
Zakaria waweza kuwa umeanza kwa wazo la nje la kuokoa la Kimasiha. Hata hivyo
wazo hili laonyesha kwenda mbali zaidi ya kile kisemwacho katika utenzi huu.
Tunaweza kujifunza kutoka ‘kuhani-nabii,’ ambaye hali hii inatabiri juu ya watu
wale wenye hekima, ‘mamajusi’ na kuleta sadaka zao kwa Kristo ambaye bado kuzaliwa. Tendo hilo pia
linatoa tafsi ya “nini kuhusu wokovu wa kikristo,” na “kwa nini unatolewa
kwetu.”
Kuna kitu ambacho kipo
wazi na hai kuhusu mtoto ambaye ameweka yote
yasiyojulikana katika mikono ya mama yake. Tofauti kati ya yeye kama
yeye na kazi ambayo inamsubiri, ubaba wa ajabu na furaha ambayo bado kueleweka
juu ya mtoto, na dhana yake katika miaka ijayo, na kwenda kama mpiga mbiu-mbele
ya Bwana inajidhihirisha. Hivyo ni vyema kufahamu uzito wa ufahamu wa kinabii
katika kazi ya Yohana. Yohana Mbatizaji 'aliandaa njia' kwa kufundisha kwamba
'ukombozi' wa kweli ambao hukuwa kwa kupatikana tu ukombozi kutoka dola Kirumi,
bali pia 'ondoleo la dhambi.' “Nawe, mtoto, utaitwa nabii wake Aliye
juu, Kwa maana utatangulia mbele za uso wa Bwana umtengenezee njia zake; Uwajulishe
watu wake wokovu, Katika kusamehewa dhambi zao,” Lk 1:76.
Hivyo Yohana Mbatizaji hakutoa
tu 'maarifa ya wokovu,' katika maana ya kutatolewa kwa wokovu huo, bali pia kwa
maana ya ufahamu wa nini kuhusu wokovu huo au kinachojumuisha maana nzima ya
wokovu. Yohana Mbatizaji hakuwa mhubiri wa uasi, kama misukosuko na machafuko
kama wazalendo wa siku zake walivyokuwa wakipendelea yeye afanye, bali alikuwa
mhubiri wa toba ya kweli. Kazi yake ilikuwa kuamsha ufahamu kuhusu dhambi, na
hivyo kuwasha tamaa ya kweli juu ya wokovu na ukombozi kutoka dhambi, ambayo
ndiyo utumwa uliowatumikisha watu. Zakaria ' asiye na lawama' aliona utumwa wa
kweli ulioutumikisha Taifa lake, na nini maana ya kazi ya wokovu ikiwa ni
pamoja na kauli mbiu yake. Tunahitaji daima kukumbushwa ukweli kwamba wokovu wa
pekee na ukombozi ambayo unaweza kutufanya sisi kuwa wema unahusu kuondokana na
hali ya dhambi kwa msamaha na kwa
utakatifu, na hivyo kutoka katika kongwa la dhambi.
Maneno yanayoufunga
utenzi huu wa Zakaria, “Kuwaangaza wakaao katika giza na uvuli wa mauti, Na
kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani,” Lk 1:79, yafungua baraka na neema
kwa watu wote wenye hofu ya Mungu na wanaoishi katika kweli na haki. Hivyo kumjua
Mungu kupitia marafiki zetu, ni pamoja
na kupatanishwa nao kwa hali zote. Kuwa rafiki ya watu wote, ni amani. Hivyo
njia ya kuelekea heri hiyo inaonyeshwa kwetu kwa jua la haki ambao upendo wa
moyo wa Mungu ametumwa katika kuleta mwanga.
Hakuna shaka kwamba Zakaria anaona kwa undani zaidi ukombozi ambao
Kristo angeuleta kuliko kuvunjwa kwa ukomo wa kifungo cha kidunia.
Tumsifu Yesu Kristo!
“Bwana ni nguvu zangu, na wimbo
wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu
wa baba yangu, nami nitamtukuza,” Kut 15:2
Tusali:-Ee
Yesu na Mkombozi wetu, tuongoze mara zote katika mwanga wako. Amina
No hay comentarios:
Publicar un comentario