JUMAMOSI WIKI
YA 32 YA MWAKA-B
14/11/2015
Somo: Hek
18:14-16; 19:6-9
Zab: 105:2-3,
36-37, 42-43
Injili: Lk
18:1-8
Nukuu:
“Neno lako Mwenyezi alishuka mbinguni kutoka
kiti chako cha kifalme, shujaa aliye hodari, katika nchi iliyopasishwa hukumu,
mwenye upanga mkali, ndio amri yako isiyopindika,”Hek 18:15
“Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu, lakini, kwa kuwa mjane huyu
ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima,” Lk
18:4b-5
“Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia
mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?” Lk
18:7
“Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja
Mwana wa Adamu, je!Ataiona imani duniani?” Lk
18:8
TAFAKARI: “Unaweza kutoa
bila kupenda, ila uwezi kupenda bila kutoa.”
Wapendwa wana wa Mungu, kuumbwa kwetu
wanadamu halikuwa hitaji la Mungu, bali kwa upendo wake alichakugua kutuumba
kwa sura na mfano wake. Kwa hiyo lengo la kwanza la uumbaji wetu ni kuishi
milele. Kwa tendo hili ni wazi kwamba lengo la pili la uumbaji wetu ni kuwa na
mahusiano na Mungu na sisi kwa sisi. Mahusiano haya msingi wake ni upendo. “Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa
mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu,” 1Kor 13:3. Kadhi
kama tulivyosoma na kusikia Injili ya leo anampa mama mjane haki yake si kwa
kupenda bali kwa kulazimika kutoka na usumbufu. Naye anasema, “Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu, lakini, kwa kuwa mjane huyu
ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima,” Lk
18:4b-5. Hivyo unaweza kutoa bila kupenda.
Tunapokuwa na mahusiano mazuri na Mungu kamwe hawezi
kutuacha katika mahangaiko yetu. Bwana wetu Yesu Kristo anatupatia uhakikisho
huyo. “Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake
wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?” Lk 18:7. Uvumilivu wa Mungu kwetu ni Imani ile
tuliyo nayo juu yake. Kwa imani dhabiti tunauhakika kwa kuyapata yale
tumwombayo Mungu wetu aliye huruma na upendo. Yesu anatupa pia uhakika wa jambo
hili, ila imani ni moja ya kielelezo kikuu kwa kile tuombacho. Nawaambia,
atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani
duniani?” Lk 18:8. Je, unayoimani kwa hayo
uyaombayo?
Kwa upande mwingine uwezi kupenda bila kutoa. Yesu anasema, “Mimi
ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo,”
Yoh 10:11. Yesu kwa kutupenda yupo tayari kutua uhai wake kwa anjili yetu.
Upendo ndiyo amri yenyewe. Kristo ndiye kielelezo chetu juu ya upendo na
kupenda. Hili ndilo lile neno lililofanyika mwili nalo likakaa kwetu. “Neno lako
Mwenyezi alishuka mbinguni kutoka kiti chako cha kifalme, shujaa aliye hodari,
katika nchi iliyopasishwa hukumu, mwenye upanga mkali, ndio amri yako
isiyopindika,”Hek 18:15. Katika mahusiano haya ayapendayo Mungu, tunaweza kuona
pia hata katika amri kuu za Mungu. Amri nne kati ya zile kumi ni uhusiano wa
mtu na Mungu. Na zile sita zilizobaki ni uhusiano wa mtu na mtu. Tumpende Mungu
na tuwapende watu, na sote tupendane.
Tumsifu Yesu Kristo!
“Yeye asiyependa,
hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo,” 1Yoh 4:8
No hay comentarios:
Publicar un comentario