ALHAMISI WIKI YA 34 YA MWAKA-B
26/11/2015
Somo: Dan 6:12-28
Zab: Dan 3:68, 69, 70, 71, 72, 73, 74
Injili: Lk 21:20-28
Nukuu:
“Mungu wangu amemtuma malaika wake, naye ameyafumba makanwa ya
simba, nao hawakunidhuru; kwa kuwa mbele zake mimi nalionekana kuwa sina hatia;
tena, mbele yako, Ee mfalme, sikukosa neno,” Dan 6:22
“Basi mfalme akafurahi sana, akaamuru wamtoe Danielii katika
lile tundu. Ndipo Danielii akatolewa katika lile tundu, wala dhara lo lote
halikuonekana mwilini mwake, kwa sababu alikuwa anamtumaini Mungu wake,” Dan
6:23
“Mfalme akaamuru, nao wakawaleta wale watu waliomshitaki
Danielii, wakawatupa katika tundu la simba, wao, na watoto wao, na wake zao; na
wale simba wakawashinda wakaivunja mifupa yao vipande vipande, kabla hawajafika
chini ya tundu,” Dan 6:24
“Ndipo mfalme Dario akawaandikia watu wa kabila zote, na taifa
zote, na lugha zote, waliokaa juu ya uso wa dunia; Amani na iongezeke kwenu,”
Dan 6:25
“Mimi naweka amri, ya kwamba katika mamlaka yote ya ufalme
wangu watu watetemeke na kuogopa mbele za Mungu wa Danielii; maana yeye ndiye
Mungu aliye hai, adumuye milele, na ufalme wake ni ufalme usioharibika, na
mamlaka yake itadumu hata mwisho,” Dan 6:26
“Yeye huponya na kuokoa, hutenda ishara na maajabu mbinguni na
duniani, ndiye aliyemponya Danielii na nguvu za simba,” Dan 6:27
“Basi Danielii huyo akafanikiwa katika enzi ya Dario, na
katika enzi ya Koreshi, Mwajemi,” Dan 6:28
“watu wakivunjika
mioyo kwa hofu, na kwa kutazamia mambo yatakayoupata ulimwengu. Kwa kuwa nguvu
za mbinguni zitatikisika,” Lk 21:26
“Hapo ndipo
watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika wingu pamoja na nguvu na utukufu
mwingi,” Lk 21:27
“Basi mambo hayo
yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu
umekaribia,” Lk 21:28
TAFAKARI: “Kiama kina hofu kwa wale wasio mwamini Mungu aliye Hai.”
Wapendwa wana wa Mungu, habari za mwisho wa nyakati
zinawatisha wengi na hasa wale wasio mwamini Mungu aliye hai. Maisha hujawa na
hofu kwa sababu ya kuishi kwa kubahatisha bahatisha. Hofu huwa tishio kubwa
zaidi pale mtu anapokosa msingi imara wa maisha yake. “Watu wakivunjika
mioyo kwa hofu, na kwa kutazamia mambo yatakayoupata ulimwengu. Kwa kuwa nguvu
za mbinguni zitatikisika,” Lk 21:26. Pamoja na
hayo yote tunahitaji kuishinda hofu. Nabii Danieli anaishinda hofu yake kwa
sababu anamsingi imara wa Imani yake. Imani yake ipo kwa Mungu aliye hai. Hivyo
maagizo ya mfalme Dario kwamba sala zote zielekezwe kwake na siyo kwa Mungu,
Danieli anapinga jambo hilo na anazidi kuomba kwa Mungu wake aliye hai. Kosa la
kwenda kinyume cha maagizo ya mfalme ilikuwa kutupwa katika tundu la simba na
kuliwa hadi kwisha. Hata pamoja na ukatili huo, Danieli Nabii hakuogopa kwa
sababu alijua ni nani anayemtumikia, Mungu aliye hai.
Baada ya kutupwa kwenye tundu la simba kwa kukaidi amri ya
mfalme, Danieli hakudhurika na simba wale. Danieli anasema, “Mungu wangu amemtuma malaika wake, naye
ameyafumba makanwa ya simba, nao hawakunidhuru; kwa kuwa mbele zake mimi
nalionekana kuwa sina hatia; tena, mbele yako, Ee mfalme, sikukosa neno,” Dan
6:22. Mungu hufanya njia pasipo njia hasa kwa
wale wanaomtumaini kila wakati. Ni kweli kwamba pamoja na sheria ile mfalme
hakutaka kuitekeleza kwa Danieli kwa sababu alimjua Danieli kuwa ni mtu wa
Mungu. Mfalme alilazimika kufanya vile kwa shinikizo la watu, na hakuweza
kupinga kwa sababu ‘sheria ni msumeno.’ Hata hivyo mfalme hakuacha kuizuia
furaha yake alipomwana Danieli mzima licha ya kukaa kwenye tundu la simba kwa
usiku mzima. “Basi mfalme akafurahi sana, akaamuru wamtoe Danielii katika
lile tundu. Ndipo Danielii akatolewa katika lile tundu, wala dhara lo lote
halikuonekana mwilini mwake, kwa sababu alikuwa anamtumaini Mungu wake,” Dan
6:23. Tendo hili linaamsha hasira kwa wale walimfitini Danieli kwa mfalme. “Mfalme akaamuru, nao wakawaleta wale watu waliomshitaki
Danielii, wakawatupa katika tundu la simba, wao, na watoto wao, na wake zao; na
wale simba wakawashinda wakaivunja mifupa yao vipande vipande, kabla hawajafika
chini ya tundu,” Dan 6:24. Ni vyema mara
nyingi tukashughulikia maisha na utakatifu wetu, badala ya kuangaika na mambo
ya watu wengine. Ona sasa malipo ya wale wafitini wa Danieli. “Mfalme
akaamuru, nao wakawaleta wale watu waliomshitaki Danielii, wakawatupa katika
tundu la simba, wao, na watoto wao, na wake zao; na wale simba wakawashinda wakaivunja
mifupa yao vipande vipande, kabla hawajafika chini ya tundu,” Dan 6:25. Kati yetu wapo watu kazi yao kubwa kutwa
nzima ni kuripoti matukio yasiyo rasmi. Kuripoti matukio yasiyo rasmi na yasiyo
na vielelezo hujulikana kama umbea.
Udhihirisho
wa Mungu aliye hai kupitia tukio hili la Danieli kutokuliwa na simba, linakuwa
wokovu kwa mfalme Dario na ukurasa mpya kwa watu wake. Kwa msimamo imara wa
Imani wa Danieli unakuwa ufumbuzi wa tatizo kwa wengi, na wote wanaishi kwa
amani na furaha. Mfalme Dario anasema, “Mimi naweka amri, ya kwamba katika mamlaka yote ya ufalme
wangu watu watetemeke na kuogopa mbele za Mungu wa Danielii; maana yeye ndiye
Mungu aliye hai, adumuye milele, na ufalme wake ni ufalme usioharibika, na
mamlaka yake itadumu hata mwisho,” Dan 6:26. Kumbe kusimama katika kweli hata
kama kweli hiyo imezungukwa na mazingira hatarishi mwisho wake huwa mzuri.
Hivyo hakuna mwenye mamlaka ya kuchukuwa maamuzi yako kama waona yapo sawa na
yaliyo simama katika kweli na haki. Mungu
huyu aliye wa kweli na hai hawezi mtupa mja wake. “Yeye huponya na kuokoa, hutenda ishara na
maajabu mbinguni na duniani, ndiye aliyemponya Danielii na nguvu za simba,” Dan
6:27. Danieli anatufundisha kusimama katika kweli. Kilicho cheusi na kisemwa
kama kilivyo cheusi na kilicho cheupe kisemwe hivyo hivyo kama kilivyo, hata
kama mazingira ya kusema hivyo ni hatarishi. Ni kupitia wewe tu Mungu
atajidhihirisha kwako na kuwa faida kwako na kwa wengine. “Basi Danielii huyo akafanikiwa katika enzi ya
Dario, na katika enzi ya Koreshi, Mwajemi,” Dan 6:28. Mafanikio ya Mtu ni tokeo
la uthubutu wake kwa yale yanayoonekana magumu na yasiyowezekana.
Mungu huyu aliye hai anaonekana katika uhalisia wake kupitia
kazi za Mwanaye Yesu Kristo kama mkombozi. Huyu ndiye aliyetumwa kukomboa kile
kilicho anguka kwa sababu ya dhambi. Pamoja na mambo mengi ya kutisha kutokana
na mwisho wa nyakati na hasa kuharibiwa kwa hekalu la Yerusalema na watu wake
kuteswa na kupelekwa utumwani, Mungu hata acha kamwe kuonyesha nguvu na utukufu
wake. “Hapo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika wingu
pamoja na nguvu na utukufu mwingi,” Lk 21:27. Hii ndiyo itakayokuwa ishara ya
mwisho kwetu kuhusu mwisho wa nyakati. “Basi mambo hayo
yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu
umekaribia,” Lk 21:28. Huu ni ule ukombozi wa siku ya mwisho, licha kweli kwamba kila siku tumepewa ya ukombozi
huo.
Basi
ndugu yangu tutumie fursa tunazopewa na Mama Kanisa kila siku na hasa kupitia
masakramenti yake ili tupata wokovu huo. Kiama
kina hofu kwa wale wasio mwamini Mungu aliye hai.
Tumsifu
Yesu Kristo!
“Bwana huua, naye
hufanya kuwa hai; Hushusha hata kuzimu, tena huleta juu. Bwana hufukarisha mtu, naye
hutajirisha; Hushusha chini, tena huinua juu,” 1Sam 2:6-7
No hay comentarios:
Publicar un comentario