JUMAMOSI
WIKI YA 14 YA MWAKA-C
Somo: Isa 6:1-8
Zab: 93:1ab, 1cd-2, 5
Injili: Mt 10:24-33
Nukuu:
“Ndipo niliposema,
Ole wangu! Kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu,
nami ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona
Mfalme, Bwana wa majeshi,” Isa 6:5
Kisha
mmoja wa maserafi wale akaruka akanikaribia; naye alikuwa na kaa la moto
mkononi mwake, ambalo alikuwa amelitwaa kwa makoleo toka juu ya madhabahu; akanigusa kinywa changu kwa kaa hilo,
akaniambia, Tazama, hili limekugusa midomo yako, na uovu wako umeondolewa, na
dhambi yako imefunikwa,” Isa 6:6-7
“Kisha nikaisikia
sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili
yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi,” Isa 6:8
“Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu,
nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni. Bali mtu ye yote atakayenikana mbele
ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni,” Mt 10:32-33
TAFAKARI: “Niwaambialo ninyi katika giza,
lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu ya nyumba.”
Wapendwa wana wa Taifa la Mungu, wito
wa Nabii Isaya unaonyesha mtazamo wa Mungu na jinsi tunavyojitazama kama watu
tusiostahili kwa yale Mungu anayotufikiria. Hakika upendo, huruma, msamaha,
haki, na upole wa Mungu hatuwezi kuufananisha na kitu chochote. Mungu atabaki
kuwa Mungu kwa milele yote! Isaya anapotazama mwaliko wa Mungu na kile alicho
anaona ni vitu viwili tofauti. Naye anasema, “Ole
wangu! Kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami
ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme,
Bwana wa majeshi,” Isa 6:5. Pamoja na historia zetu zilizombaya, kushindwa
kwetu katika maisha, na kudharauliwa kwetu, bado Mungu anasema, “Niwaambialo
ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu
ya nyumba,” Mt 10:27. Tuitazamapo historia ya wokovu wetu, ipo mifano mingi na
mazingira mbalimbali ambapo Mungu ukiinua kile kilicho dhaifu na kunyenyekeza
kile kinachojikuza.
Mungu
hutumia watu wa kawaida kabisa kulifikia lengo lake Takatifu. Nabii Isaya ni
mmoja wapo, hasa anapojitazama mazuri na mabaya yake. Bila shaka mimi na wewe
tunajisikia kama Nabii Isaya. Mapungufu na udhaifu wewe visiwa ukuta wa kuona
nuru ya Mungu. Tusimame katika kweli na haki hata kama udhaifu upo. Huku ni
kuishi maisha ya ufufuko, yaani, “mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo,
yatafuteni yaliyo juu Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu,” Kol 3:1.
Hivyo, udhaifu wangu uwe changamoto na nguvu ya kunisukuma kufanya vizuri zaidi
siku kwa siku. Na hii ndiyo maana ya maneno haya ya Mtume Paulo kwamba,
“napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya
Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu,” 2Kor 12:10. Kumbe katika
hali zote na udhaifu wangu, Kristo awe kielelezo changu cha kufanya vizuri
zaidi. Yeye kesha ushinda Msalaba.
Ndugu
yangu tunayesafiri sote katika tafakari hii, ‘tuambiwalo
katika giza, tuliseme katika nuru; na tusikialo kwa siri, tulihubiri juu ya
nyumba.’ Neno hili la maanisha hivi; pamoja na ‘shindwa yako bado
una kitu cha kufanya na kubadili historia yako mbaya. Hivyo kitumie kitu hicho
katika ukamilifu wake na hadi mwisho wake, na yote yatakuwa mapya.’ Huu ndiyo
ujumbe mahususi.
Mpendwa
katika Kristo, unapojiachia kwa Mungu bila kujibakiza katika maana ya kuona
kweli kama ilivyo na siyo kama ulivyo, ndipo utakaso unapokujilia na kufanywa
upya mbele ya Mungu, na kuhesabiwa haki kwa mastahili ya Mungu mwenyewe. Isaya
anayaendea mabadiliko haya katika maisha yake kwa sababu Mungu kesha pendezwa
naye. “Kisha mmoja wa maserafi wale akaruka
akanikaribia; naye alikuwa na kaa la moto mkononi mwake, ambalo alikuwa
amelitwaa kwa makoleo toka juu ya madhabahu; akanigusa
kinywa changu kwa kaa hilo, akaniambia, Tazama, hili limekugusa midomo yako, na
uovu wako umeondolewa, na dhambi yako imefunikwa,” Isa 6:6-7. Ni mara ngapi
tunajiona watu tusiofaa mbele za watu na kujipoteza kabisa? Ndugu yangu, hata
kama ulimwengu wote utakuchukia, Mungu hubaki na upendo wake kwako wa ajabu.
Embu itazame mikono ya Yesu pale msalabani. Yesu anakuambia, ‘tazama nimeyakubali
haya yote na hata kufa kifo cha aibu msalabani kwa sababu nakupenda kupita
vyote.’ Hakika Mungu anatupenda upeo,
Yoh 13:1.
Wapendwa wana wa Mungu,
utaisikia sauti ya Mungu ndani yako unapo utafakari upendo huu wa Mungu ulio wa
ajabu. Isaya anaisikia sauti ya Mungu ndani yake, na kusema, “Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye
ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume
mimi,” Isa 6:8. Isaya anazaliwa upya mwili na roho na sasa yupo tayari
kuyafanya mapenzi ya Mungu. Huwezi kukutana na Mungu katika maisha yako naye
akakuacha kama ulivyokuwa mwanzo.
Ndugu yangu, unapomfuata Kristo kwa ukaribu, unakumbushwa
kuishinda hofu na woga. Unayepaswa kumwogopa ni Mungu mwenyewe. “Basi, msiwaogope, kwa maana hakuna neno
lililositirika, ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa, ambalo
halitajulikana,” Mt 10:26. Ndugu yangu, hata
kama leo tutafinywa uhuru wetu tunapoishi imani yetu, kweli hiyo ipo siku
itajulikana wazi kwa watesi wetu. “Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali
mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum,” Mt 10:28
Tunapolishinda giza kwa matendo yetu ya mwanga, kutatutaka
kila mara kusimama katika kweli na kumshuhudia Kristo pasipo haya. “Basi, kila
mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye
mbinguni. Bali mtu ye yote
atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye
mbinguni,” Mt 10:32-33. Maisha yetu na ukiri wetu mbele za watu kuhusu Kristo
ndiyo kweli hiyo itakayo jidhihirisha mbele za Mungu siku ya hukumu ya mwisho.
Tumsifu Yesu Kristo!
“Ndipo
niliposema, Mimi hapa, nitume mimi,” Isa 6:8b
Tusali:-Ee Yesu Mwema,
nitazama na kunipa nguvu hata katika udhaifu wangu. Amina
No hay comentarios:
Publicar un comentario