JUMANNE WIKI YA 1 YA MWAKA-C
12/1/2016
Somo: 1Sam 1:9-20
Zab: 1Sam 2:1, 4-7,
8abcd
Injili: Mk 1:21-28
Nukuu:
“Akaweka nadhiri, akasema, Ee Bwana wa majeshi, ikiwa wewe
utaliangalia teso la mjakazi wako, na kunikumbuka, wala usinisahau mimi mjakazi
wako, na kunipa mimi mjakazi wako mtoto mume, ndipo mimi nitakapompa Bwana huyo
mtoto siku zote za maisha yake, wala wembe hautamfikilia kichwani kamwe,” 1Sam
1:11
“Ndipo Eli akajibu, akasema, Enenda kwa amani; na Mungu wa
Israeli akujalie haja yako uliyomwomba,” 1Sam 1:17
“Naye akasema, Mjakazi wako na aone kibali machoni pako. Basi
huyo mwanamke akaenda zake, naye akala chakula, wala uso wake haukukunjamana
tena,” 1Sam 1:18
“Wakaondoka asubuhi na mapema, wakasali mbele za Bwana, kisha
wakarejea na kufika nyumbani kwao huko Rama; Elkana akamjua mkewe Hana; naye
Bwana akamkumbuka,” 1Sam 1:19
“Ikawa, wakati ulipowadia, Hana akachukua mimba na kuzaa mtoto
mwanamume; akamwita jina lake Samweli, akisema, Kwa kuwa nimemwomba kwa Bwana,”
1Sam 1:20
“Wakashangaa mno kwa mafundisho yake; kwa maana alikuwa
akiwafundisha kama mtu mwenye amri, wala si kama waandishi,” Mk 1:22
“Na mara palikuwapo ndani ya sinagogi lao mtu mwenye pepo mchafu;
akapaza sauti, akisema, Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je! Umekuja
kutuangamiza?” Mk 1:23-24
“Nakutambua u nani, Mtakatifu wa Mungu. Yesu akamkemea, akisema,
Fumba kinywa, umtoke,” Mk 1:25
“Wakashangaa wote, hata wakaulizana, wakisema, Nini hii? Ni elimu
mpya! Maana kwa uweza awaamuru hata pepo wachafu, nao wamtii!” Mk 1:27
TAFAKARI: “Hakuna lisilowezekana kwa Mungu. Kuwa na Imani.”
Wapendwa wana wa Mungu,
Mungu wetu sio Mungu wa kushindwa hata kidogo. Kwa maneno mengine, Mungu
ninaye mwamini hawezi kuliumba jiwe kubwa kiasi chochote kile unachoweza
kufikiria alafu ashindwe kulibeba jiwe hilo. Huyo siye Mungu ninayemwamini! Je,
waamini Mungu anaweza?
Kwa imani aliyokuwa nayo Hana na nadhiri aliyoweka juu ya
mtoto yule aliyemwomba Mungu, yote yanatendeka. Nadhiri awekayo mtu kwa kile
aombacho ndiyo dhamiri ibebayo kile aombacho. Mara nyingi tunaomba na hatupati
kwa sababu dhamiri iliyondani yako ni mbaya hata kama kile uombacho kwa mtazamo
wa nje ni kizuri. Na hii ndiyo sababu anayotupa Mtume Yakobo kwa nini
hatujibiwi maombi yetu. “Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie
kwa tamaa zenu,” Yak 4:3. Dhamiri ya Hana kwa kile aombacho ni njema na nzuri
machoni mwa Mungu. Hana “Akaweka nadhiri, akasema, Ee Bwana wa majeshi, ikiwa wewe
utaliangalia teso la mjakazi wako, na kunikumbuka, wala usinisahau mimi mjakazi
wako, na kunipa mimi mjakazi wako mtoto mume, ndipo mimi nitakapompa Bwana huyo
mtoto siku zote za maisha yake, wala wembe hautamfikilia kichwani kamwe,” 1Sam
1:11
Hata hivyo Mungu hutumia mambo yale yale ya kawaida kadiri
ya hali zetu, mazingira na uwezo wetu kutenda Makuu yake wetu tunapojiachia
kwake pasipo shaka. Hivyo, Eli Kuhani, alipowapa baraka Hana na Mumewe, “wakaondoka asubuhi na
mapema, wakasali mbele za Bwana, kisha wakarejea na kufika nyumbani kwao huko
Rama; Elkana akamjua mkewe Hana; naye Bwana akamkumbuka,” 1Sam 1:19. Ikiwa
uliweka nadhiri kwa Mungu na ukafanikiwa kile ulichokiomba, yakupasa kufanya
kadiri na ahadi yako. “Ikawa, wakati ulipowadia, Hana akachukua mimba na kuzaa mtoto
mwanamume; akamwita jina lake Samweli, akisema, Kwa kuwa nimemwomba kwa Bwana,”
1Sam 1:20.
Wapendwa
wana wa Mungu, uwepo wa Kristo katika maisha yetu umetuweka karibu sana na
Mungu naye ndiye Mungu. Alitamkalo Yesu limejaa mamlaka yote kwani ni neno
aliyemwilishwa. “Wakashangaa mno kwa mafundisho yake; kwa maana alikuwa
akiwafundisha kama mtu mwenye amri, wala si kama waandishi,” Mk 1:22.
Litamkwapo jina la Yesu hakuna nguvu yoyote ile na hasa nguvu za giza
zinazoweza kustahimili jina hili Tukufu kupita majina yote. “Na mara palikuwapo ndani
ya sinagogi lao mtu mwenye pepo mchafu; akapaza sauti, akisema, Tuna nini nawe,
Yesu wa Nazareti? Je! Umekuja kutuangamiza?” Mk 1:23-24. Nguvu na Utukufu wa
Kristo hata pepo wachafu wanajua na kukiri. “Nakutambua u nani, Mtakatifu wa Mungu. Yesu akamkemea, akisema,
Fumba kinywa, umtoke,” Mk 1:25.
Nguvu na
Mamlaka aliyo nayo Kristo Yesu, hakuna chochote tutakachomwomba kwa imani na
dhamiri njema aache kutupatia. Na yote hayo huyafanya kadiri ya mapenzi yake na
mahitaji yetu. “Ndiye Mungu mwenye hekima peke yake. Utukufu una yeye kwa Yesu
Kristo, milele na milele. Amina,” Rum 16:27. Ukweli huu unathibitika ndani ya
sinagogi alivyokinyamazisha kichwa cha pepo mchafu na kuamuru amtoke mtu yule. “Wakashangaa wote, hata
wakaulizana, wakisema, Nini hii? Ni elimu mpya! Maana kwa uweza awaamuru hata
pepo wachafu, nao wamtii!” Mk 1:27. Hakuna
lisilowezekana kwa Mungu. Kuwa na Imani.
Tumsifu Yesu Kristo!
“Kwa kuwa vitu vyote
vyatoka kwake, viko kwa uweza wake, tena vinarejea kwake. Utukufu una yeye
milele. Amina,” Rum 11:36
No hay comentarios:
Publicar un comentario