JUMATATU YA WIKI 4 YA KWARESMA
Somo:
Isa 65:17-21
Zab:
30:1, 3, 4-5, 10-11a, 12b
Injili:
Yoh 4:43-54
Nukuu:
“Maana, tazama, mimi
naumba mbingu mpya na nchi mpya, na mambo ya kwanza hayatakumbukwa, wala
hayataingia moyoni,” Isa 65:17
“Yesu mwenyewe
alishuhudia ya kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe. Basi Yesu
akamwambia, “Msipoona ishara na maajabu hamtaamini kabisa?””, Yoh 4:44,48.
TAFAKARI:
“Mara zote Mungu huanza upya na watu wake; Kristo Yesu ndiye ufunuo halisi wa
utimilifu huo wa Mungu”
Wapendwa wana wa Mungu,
“Mara zote Mungu huanza upya na watu wake; Kristo Yesu ndiye ufunuo halisi wa
utimilifu huo wa Mungu.” Nabii Isaya katika somo letu la leo anaelezea furaha
hiyo ya Mungu kuanza upya na watu wake baada ya kuyaona mateso yao. “Maana,
tazama, mimi naumba mbingu mpya na nchi mpya, na mambo ya kwanza
hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni,” Isa 65:17. Mwanzo huu mpya ni pamoja
na kuwapa watu wake maisha marefu, ila watenda dhambi watalaaniwa ingawa
watafaidi kwa kuwa na umri mrefu. Kwa namna nyingine, mafanikio yetu pasipo
Mungu si kidhibitisho cha kufaulu kwetu. Amani ya kweli upatikana pale
tunapomuhusisha Mungu yote tufanyayo.
Utimilifu huu wa kazi
ya Mungu ya kuanza upya na watu wake inajidhihisha ndani ya mwanaye, yaani,
Yesu Kristo. Ishara za Yesu Kristo zadhihirisha utimilifu wa ahadi ya Mungu
kuanza mpya na watu wake. Jambo hili liliwekwa wazi siku ya kugeuka sura kwa
Bwana wetu Yesu Kristo. “Alipokuwa katika kusema, wingi jeupe likawatia uvuli;
na tazama, sauti ikatoka katika like wingu, ikasema, Huyu ni Mwangu, mpendwa
wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye,” Mt 17:5. Je, waamini maneno hayo?
Ndugu yangu ule Mkristo,
kufanikiwa kwetu kiimani, ikiwa ni kuanza yote upya kuelekea maisha ya umilele,
mpango huu unawezekana tu kwa njia ya Yesu na ndani ya Yesu. Kinachoongoza
safari hii ya kiimani ni Msimamo wa Imani tuliyonayo juu ya Yesu. Tunapokuwa na
imani thabiti, yote hudhihirishwa ndani yetu. Tunapokuwa na imani Mungu hufanya
mambo makubwa na kujidhihirisha kwetu. “Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na
imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, ondoka hapa uende kule;
nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu,” Mt 17:20. Ukristo
bila Kristo ni sawa na samaki kutamani kuishi jangwani.
Kwa njia ya Imani hii, leo
tunaona uponyaji wa mtoto wa diwani. Kwa kuiona imani hii, Yesu anamwambia,
“Enenda; mwanao yu hai.” Yoh 4:50. Ila tunapewa angalizo na changamoto katika
swala la Imani. Tusiamini tu kwa sababa ya kuziona Ishara. Imani ya kweli
haiitaji Ishara. Ila tunapoamini kweli, Mungu ujidhihirisha ndani ya kile
tunachoamini. Kwa jambo hili Yesu anasema, “Msipoona ishara na maajabu
hamtaamini kabisa?” Yoh 4:48. Ishara si kigezo cha Imani. “Basi imani ni kuwa
na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana,” Ebr 11:1.
Ndugu yangu, tusisahau
kwamba, “kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata
vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri,” Ebr 11:3. Na ni kwa
njia hii ya imani yote yawezekana katika Yesu Kristo Kristo, ambaye yeye
twapaswa kumwamini na kumsikiliza kila wakati.
Kwa nini basi ndugu
yangu kila siku unahama makanisa na vikundi vya kitume tutafuta ishara?
Tumsifu Yesu Kristo!
“…Kizazi
hiki ni kizazi kibaya; kinatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya
Yona. Maana, kama vile Yona
alivyokuwa ishara kwa Waninawi, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu kwa kizazi
hiki,” Lk 11:29-30
Tusali:-Ee
Yesu na Mkombozi wetu, twaamini yote yanawezekana ndani yako na kwa njia yako.
Amina.
No hay comentarios:
Publicar un comentario