JUMATATU WIKI YA 5 YA MWAKA-C
Somo:
1Fal 8:1-7, 9-13
Zab:
132:6-7, 8-10
Injili:
Mk 6:53-56
Nukuu:
“Hamkuwa na kitu ndani ya sanduku, ila zile mbao mbili za mawe
ambazo Musa aliziweka ndani huko Horebu, Bwana alipofanya agano na wana wa
Israeli, hapo walipotoka katika nchi ya Misri,” 1Fal 8:9
“Ikawa, makuhani walipotoka katika patakatifu, nyumba ya Bwana
ikajaa wingu; hata makuhani
hawakuweza kusimama ili kufanya huduma yao, kwa sababu ya wingu lile; kwa kuwa
nyumba ya Bwana ilikuwa imejaa utukufu wa Bwana,” 1Fal 8:10-11
“Ndipo Sulemani akanena, Bwana alisema ya kwamba atakaa katika
giza nene,” 1Fal 8:12
“Hakika nimekujengea nyumba ya kukaa, iwe mahali pa makao yako
milele,” 1Fal 8:13
“wakaenda mbio,
wakizunguka nchi ile yote, wakaanza kuwachukua vitandani walio hawawezi, kwenda
kila mahali waliposikia kwamba yupo,” Mk 6:55
“Na kila alikokwenda,
akiingia vijijini, au mijini, au mashambani, wakawaweka wagonjwa sokoni,
wakamsihi waguse ngaa pindo la vazi lake; nao wote waliomgusa wakapona,” Mk
6:56
TAFAKARI:
“Nyakati za uwepo wa Mungu na Utukufu wake.”
Wapendwa wana wa Mungu,
vyote vinavyooneka na visivyoonekana vya udhihirisha uwepo wa Mungu na utukufu
wake. Ila kwa namna ya pekee uwepo wako na wangu licha ya kuudhihirisha uwepo
na Utukufu wa Mungu, kwa kulitambua jambo hili na KUMRUDISHIA Utukufu huo
Mungu, ni furaha kubwa kwa Mungu na baraka wetu. Hatua ya kwanza, yaani,
“kutambua” wajibu huu muhimu [“KURUDISHA”] ni kufahamu kuwa uwepo wako leo kwa
namna yoyote ile si kwa sababu yako na wasi si kwa nguvu zako na uwezo wako. “Kwa sababu hakuna mtu miongoni mwetu aishiye kwa
nafsi yake, wala hakuna afaye kwa nafsi yake,” Rum 14:7. Hivyo chochote
ufanyacho kwa nia njema na katika ukamilifu wake ni kurudisha sifa na utukufu
wa Mungu, na kwa wakati huo huo unaudhihirisha uwepo wa Mungu na utukufu wake.
Ufahamu huu wa kuona
haya ya kawaida katiaka maana isiyo ya kawaida katika mtazamo wa Kimungu ndiyo
tofauti kubwa iliyopo kati ya mwenye kujua nyakati za uwepo wa Mungu na Utukufu wake [kinadharia],
na yule mwenye kuamini na kuishi
uwepo huo wa Mungu na Utukufu wake. Ndugu yangu, katika mtazamo na ufahamu huu
wa Kimungu kamwe haijalishi ni aina gani ya kazi halali kwa malipo mahali
unayoifanya. Vile vile haijalishi ni kiwango gani cha elimu ulicho nacho, na
dhamana gani uliyopewa na umma. Ukweli ni kwamba, sababu kubwa ya ukifanyacho
husukumwa na HOFU YA MUNGU. Ni kwa wale tu waliofikia hatua hii ya maisha ya
kiroho na uweza pamoja na Mtume Paulo, “Kwa
maana kama tukiishi, twaishi kwa Bwana, au kama tukifa, twafa kwa Bwana. Basi
kama tukiishi au kama tukifa, tu mali ya Bwana,” Rum 14:8. Utendaji na mtazamo
wa mtu wa ngazi hii kiroho na kimaisha ni tofauti kabisa. Uwepo wa mtu huyu
popote pale alipo hudhihirisha uwepo wa Mungu na utukufu wake.
Hatua ya
pili baada ya kutambua sababu ya uwepo wako hapa duniani ambayo ni
kuudhihirisha huo utukufu na uwepo wa Mungu, ni kutimiza ahadi yako kwa wakati na kwa uaminifu mkubwa
uliyomwekea Mungu. Kumbuka ahadi
hiyo uliyoweka kwa Mungu ilikuwa ni tokea la kutendewa kwa namna ya pekee na
ajabu na Mungu kusikokuwa na mastahili yako wewe kama wewe. Hapa ni wewe na
Mungu wako. “Maana
ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo
ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa
Mungu,” 1Kor 2:11. Mfalme Sulemani katika
hili anatimiza ahadi yake ya kumjengea Mungu nyumba, na kuliweka saduku lile la
Agano kulipo salama zaidi. “Hamkuwa na kitu ndani ya sanduku, ila zile mbao mbili za
mawe ambazo Musa aliziweka ndani huko Horebu, Bwana alipofanya agano na wana wa
Israeli, hapo walipotoka katika nchi ya Misri,” 1Fal 8:9. Hata hivyo, ni kwa namna hii na mtindo huu uwepo
wa Mungu kati ya watu wake ulijidhihirisha. “Hakika
nimekujengea nyumba ya kukaa, iwe mahali pa makao yako milele,” 1Fal 8:13. Tendo hili ni furaha kwa Mungu na baraka kwa
Mfalme Sulemani.
Wapendwa
wana wa Mungu, alichokifanya Mfalme Sulemani kinadhihirisha pia uwepo wa Mungu
na utukufu wake. “Ikawa, makuhani walipotoka katika patakatifu, nyumba ya Bwana
ikajaa wingu; hata makuhani
hawakuweza kusimama ili kufanya huduma yao, kwa sababu ya wingu lile; kwa kuwa
nyumba ya Bwana ilikuwa imejaa utukufu wa Bwana,” 1Fal 8:10-11. Kile ufanyacho
kwa uaminifu katika kweli na haki umwakilisha na kumtambulisha Mungu pale
ulipo.
Hatua ya kwanza na hii ya pili, yaani katika kutambua na
kutimiza ahadi mbele ya Mungu uwezekana tu pale hayo yanaposukumwa na Imani
pasipo shaka. Ndugu yangu, utaweza kuyafanya yote bila shaka kwa vile unaamini
kile ufanyacho na kwa sababu gani unakifanya. Hili ndilo tunaloliona katika
Injili ya leo. “Wakaenda mbio, wakizunguka nchi ile yote, wakaanza kuwachukua
vitandani walio hawawezi, kwenda kila mahali waliposikia kwamba yupo, [Yesu]” Mk
6:55. Kristo Yesu ndiye kielezo halisi cha Imani, Matumaini, na Mapendo. “Simeoni akawabariki, akamwambia Mariamu mama
yake, Tazama, huyu [Kristo Yesu] amewekwa kwa kuanguka na kuinuka wengi walio
katika Israeli, na kuwa ishara itakayonenewa,” Lk 2:34. Moja ya Ishara
zilizonenewa, Isa 61:1, na kuwa mpango kazi wa Yesu, Lk 4:17-19, ni hili
lilitokea leo, yaani, “Na kila alikokwenda, akiingia vijijini, au mijini, au
mashambani, wakawaweka wagonjwa sokoni, wakamsihi waguse ngaa pindo la vazi
lake; nao wote waliomgusa wakapona,” Mk 6:56. Mungu anajidhihirisha kwa watu
wake na waja wake wenye hofu naye, na kwa wakati huo huo anaufunua Utukufu wake
kwa wale wote wanao mwamini.
Tumsifu
Yesu Kristo!
“Mtu ni
kitu gani hata umkumbuke, Na binadamu hata umwangalie? Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu;
Umemvika taji ya utukufu na heshima; Umemtawaza
juu ya kazi za mikono yako; Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake,” Zab 8:4-6
No hay comentarios:
Publicar un comentario