JUMATANO WIKI YA 22 YA MWAKA-B
Somo:
Kol: 1:1-8
Zab:
52:8-9
Injili:
Lk 4:38-44
Nukuu:
“kwa sababu ya tumaini mlilowekewa akiba mbinguni; ambalo habari
zake mlizisikia zamani kwa neno la kweli ya Injili,” Kol 1:5
“Akawaambia, Imenipasa
kuihubiri habari njema ya ufalme wa Mungu katika miji mingine pia; maana kwa
sababu hiyo nalitumwa,” Lk 4:43
TAFAKARI: “Tenda lililo jema kila siku ya maisha yako kwani ndilo
alitakalo Yesu kutoka kwetu.”
Wapendwa
wana wa Mungu, pamoja na mambo mengi tuyafanyayo leo hapa duniani, hakuna neema
na rehema nyingi tuzipatazo kwa kutenda lile lililo jema kila siku ya maisha yetu.
Tumaini letu hapa duniani hujengwa katika misingi tuliojiwekea na Kristo.
Maisha yetu yenye lengo la umilele, pasipo Kristo ni ndoto isiyokuwa na
mwelekeo kabisa. “kwa sababu ya tumaini mlilowekewa akiba mbinguni; ambalo habari
zake mlizisikia zamani kwa neno la kweli ya Injili,” Kol 1:5. Ndugu yangu
ulimwengu huu umejifungamanisha na nini?
Uwepo wa
Kristo katika maisha yetu ni habari njema ya ufalme wa Mungu. Kristo anatutaka
pamoja na mambo yote tuyafanyayo kila siku tusiache kamwe kuutafuta ufalme wa
Mungu. Ni kwa sababu hiyo Kristo kaja kwetu. Mambo yote tuyapataya duniani hapa
kwayo yenyewe siyo ukamilifu wa yale aliyotuandalia Mungu katika ufalme wake.
Yesu anawaambia wale waliokuwa wanataka kukaa naye tu, “Imenipasa kuihubiri
habari njema ya ufalme wa Mungu katika miji mingine pia; maana kwa sababu hiyo
nalitumwa,” Lk 4:43. Wapendwa, yatupasa
kuinjilishana ili kila mmoja ajue makusudi ya Yesu hapa duniani.
Tumsifu Yesu Kristo!
EE YESU TUTUMIE VYEMA
KUENEZA MAKUSUDI YAKO HAPA DUNIANI. AMIMA.
No hay comentarios:
Publicar un comentario