martes, 1 de septiembre de 2015

TAFAKARI: JUMATANO WIKI YA 22 YA MWAKA-B

JUMATANO WIKI YA 22 YA MWAKA-B
Somo: Kol: 1:1-8
Zab: 52:8-9
Injili: Lk 4:38-44
Nukuu:
kwa sababu ya tumaini mlilowekewa akiba mbinguni; ambalo habari zake mlizisikia zamani kwa neno la kweli ya Injili,” Kol 1:5
Akawaambia, Imenipasa kuihubiri habari njema ya ufalme wa Mungu katika miji mingine pia; maana kwa sababu hiyo nalitumwa,” Lk 4:43 

TAFAKARI: “Tenda lililo jema kila siku ya maisha yako kwani ndilo alitakalo Yesu kutoka kwetu.”

Wapendwa wana wa Mungu, pamoja na mambo mengi tuyafanyayo leo hapa duniani, hakuna neema na rehema nyingi tuzipatazo kwa kutenda lile lililo jema kila siku ya maisha yetu. Tumaini letu hapa duniani hujengwa katika misingi tuliojiwekea na Kristo. Maisha yetu yenye lengo la umilele, pasipo Kristo ni ndoto isiyokuwa na mwelekeo kabisa. kwa sababu ya tumaini mlilowekewa akiba mbinguni; ambalo habari zake mlizisikia zamani kwa neno la kweli ya Injili,” Kol 1:5. Ndugu yangu ulimwengu huu umejifungamanisha na nini?

Uwepo wa Kristo katika maisha yetu ni habari njema ya ufalme wa Mungu. Kristo anatutaka pamoja na mambo yote tuyafanyayo kila siku tusiache kamwe kuutafuta ufalme wa Mungu. Ni kwa sababu hiyo Kristo kaja kwetu. Mambo yote tuyapataya duniani hapa kwayo yenyewe siyo ukamilifu wa yale aliyotuandalia Mungu katika ufalme wake. Yesu anawaambia wale waliokuwa wanataka kukaa naye tu, “Imenipasa kuihubiri habari njema ya ufalme wa Mungu katika miji mingine pia; maana kwa sababu hiyo nalitumwa,” Lk 4:43. Wapendwa, yatupasa kuinjilishana ili kila mmoja ajue makusudi ya Yesu hapa duniani.

Tumsifu Yesu Kristo!


EE YESU TUTUMIE VYEMA KUENEZA MAKUSUDI YAKO HAPA DUNIANI. AMIMA.

No hay comentarios:

Publicar un comentario