JUMATATU
YA 4 YA KWARESMA
Somo:
Isa 65:17-21
Zab:
30:2, 4, 5-6, 11-12a, 13b
Injili:
Yoh 4:43-54
Nukuu:
“Maana, tazama, mimi
naumba mbingu mpya na nchi mpya, na mambo ya kwanza hayatakumbukwa, wala
hayataingia moyoni,” Isa 65:17
“Yesu mwenyewe
alishuhudia ya kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe. Basi Yesu
akamwambia, “Msipoona ishara na maajabu hamtaamini kabisa?””, Yoh 4:44,48.
TAFAKARI:
“Mara zote Mungu huanza upya na watu wake; Kristo Yesu ndiye ufunuo halisi wa
utimilifu huo wa Mungu”
Wapendwa wana wa Mungu,
“Mara zote Mungu huanza upya na watu wake; Kristo Yesu ndiye ufunuo halisi wa
utimilifu huo wa Mungu.” Nabii Isaya katika somo letu la leo anaelezea furaha
hiyo ya Mungu kuanza upya na watu wake baada ya kuyaona mateso yao. “Maana,
tazama, mimi naumba mbingu mpya na nchi mpya, na mambo ya kwanza
hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni,” Isa 65:17. Mwanzo huu mpya ni pamoja
na kuwapa watu wake maisha marefu, ila watenda dhambi watalaaniwa ingawa
watafaidi kwa kuwa na umri mrefu. Kwa namna nyingine, mafanikio yetu pasipo
Mungu si kidhibitisho cha kufaulu kwetu. Amani ya kweli upatikana pale tunapomuhusisha
Mungu yote tufanyayo.
Utimilifu huu wa kazi
ya Mungu ya kuanza upya na watu wake inajidhihisha ndani ya mwanaye, yaani Yesu
Kristo. Ishara za Yesu Kristo zadhihirisha utimilifu wa ahadi ya Mungu kuanza
mpya na watu wake. Jambo hili liliwekwa wazi siku ya kugeuka sura kwa Bwana
wetu Yesu Kristo. “Alipokuwa katika kusema, wingi jeupe likawatia uvuli; na
tazama, sauti ikatoka katika like wingu, ikasema, Huyu ni Mwangu, mpendwa
wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye,” Mt 17:5. Je, waamini maneno hayo?
Ndugu yangu, kufanikiwa
kwetu kiimani, ikiwa ni kuanza yote upya kuelekea maisha ya umilele, mpango huu
unawezekana tu kwa njia ya Yesu na ndani ya Yesu. Kinachoongoza safari hii ya
kiimani ni Msimamo wa Imani tuliyonayo juu ya Yesu. Tunapokuwa na imani
thabiti, yote hudhihirishwa ndani yetu. Tunapokuwa na imani Mungu hufanya mambo
makubwa na kujidhihirisha kwetu. “Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani
kiasi cha punje ya haradali mtauambia
mlima huu, ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno
lisilowezekana kwenu,” Mt 17:20.
Kwa njia ya Imani
hii, leo tunaona uponyaji wa mtoto wa
diwani. Kwa kuiona imani hii, Yesu anamwambia, “Enenda; mwanao yu hai.” Yoh
4:50. Ila tunapewa angalizo na changamoto katika swala la Imani. Tusiamini tu
kwa sababa ya kuziona Ishara. Imani ya kweli haiitaji Ishara. Ila tunapoamini
kweli, Mungu ujidhihirisha ndani ya kile tunachoamini. Kwa jambo hili Yesu
anasema, “Msipoona ishara na maajabu hamtaamini kabisa?” Yoh 4:48. Ishara si
kigezo cha Imani. “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni
bayana ya mambo yasiyoonekana,” Ebr 11:1.
Ndugu yangu, tusisahau
kwamba, “kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata
vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri,” Ebr 11:3. Na ni kwa
njia hii ya imani yote yawezekana katika Yesu Kristo Kristo, ambaye yeye
twapaswa kumwamini na kumsikiliza kila wakati.
Kwa nini basi ndugu
yangu kila siku unahama makanisa na vikundi vya kitume tutafuta ishara?
Tumsifu Yesu Kristo!
Kwa imani yote
yanawezekana ndani ya Yes una kwa nñjia ya Yesu. Amina.
“…Kizazi
hiki ni kizazi kibaya; kinatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya
Yona. Maana, kama vile Yona
alivyokuwa ishara kwa Waninawi, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu kwa kizazi
hiki,” Lk 11:29-30
No hay comentarios:
Publicar un comentario