JUMANNE WIKI YA 14 YA MWAKA-B
Somo: Mwa 32:22-32
Zab:16
Injili: t 9:32-38
Nukuu:
“Akamwambia,
jina lako hutaitwa tena Yokobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na
watu, nawe umeshinda,” Mwa 32:28
“Yakobo
akapaita mahali pale, Penueli, maana alisema, Nimeonana na Mungu uso kwa uso,
na nafsi yangu imeokoka,” Mwa 32:30
“Ndipo
alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache,”
Mt 9:37
“Basi
mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake,F” Mt 9:38
TAFAKARI: “Kuwa mara zote kile
ulicho.”
Wapendwa
wana wa Mungu, licha ya mapungufu yetu kama wanadamu, tunaalikwa kila siku ya
maisha yetu kuwa kile tulicho. Huwezi kusonga mbele kwa maendeleo yoyote bila
kujua kiundani kile ulicho. Siri ya mafanikio ya kila mmoja wetu ipo ndani
yetu. Mungu analithibitisha jambo hilo kwa Yakobo kwa kupata kibali mbele ya
Mungu, “Akamwambia, jina lako hutaitwa tena Yokobo, ila Israeli, maana
umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda,” Mwa 32:28. Kushinda na kupata
kibali mbele ya Mungu ni kukubaliwa na Mungu. Tunapokubaliwa na Mungu ni kwamba
tupo sehemu salama ya maisha yetu. Je, jambo hilo tunaliwekaje mbele ya macho
ya Mungu?
Yakobo
kama mwenye kupata mastahili mbele ya Mungu, yupo tayari kufanya lolote kwa
upendeleo huo. Yakobo kwa unyenyekevu yote anapaita mahali pale, “Penueli,
maana alisema, Nimeonana na Mungu uso kwa uso, na nafsi yangu imeokoka,” Mwa
32:30. Kuokoka katika maisha ni kutambua kasoro ulizokuwa nazo huko nyuma na
kuwa tayari kuanza na kuendelea na Kristo mwenye siri yote ya maisha ya sasa na
yajayo.
Wapendwa,
kila siku tunaitwa kutenda na kuishi yale yanayompendeza Mungu. Tatizo kubwa
katika ukweli huu ni kwamba hatupo tayari kuyafanya hayo. Wazo lolote lenye
kutuhitaji kufanya kile kilicho cha pekee katika maisha yetu kinaitaji kujitoa
kusipo na kipimo. Pamoja na ukweli kwamba waitwayo ni wengi, ila wanaokubali
wito huu ni wachache. Ni wachache katika maana ya kwamba nguvu na akili zetu
tuziwekazo katika utume huu hazima majibu ya haraka na mepesi. Ndipo Yesu alipowaambia wanafunzi wake, “Mavuno ni
mengi, lakini watenda kazi ni wachache,” Mt 9:37. Sote tumeitwa kuwa watendaji
wa kazi ya Mungu bia kujibakiza. Hatuwezi kuona makusudia ya Mungu juu ya
maisha yetu yanapotea bure.
Hivyo
kila siku tunaalikwa kujitoa kwa ajili ya wito Mtakatifu. Kujitoa huku ni kuwa
na dhamira chanya ya kuiombea miito mitakatifu. Tusipolifanya jambo hili kwa
ukweli na umakini wake, yote hupotea kama moshi. “Basi mwombeni Bwana wa
mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake,F” Mt 9:38. Kama wewe ni Padre
unayefanya utume wako katika parokia, ni vyema ukayatazama kwa ukaribu makundi
haya: Kuwa na wakati ujayo mwema, unapaswa kuwa karibu sana na vijana. Kuyapata
mang’amuzi ya wakati uliopita yakupasa kuwa karibu sana na wazee. Kujua
mahangaiko ya familia ya kila siku, wewe kama mchungaji na padre yakupasa kuwa
karibu sana na wazazi. Kujua furaha ya kweli, wewe kama mchungaji mwema
yakupasa kujua furaha ya kweli iliyopo kwa watoto.
Tumsifu
Yesu Kristo!
EE
YESU TAZAMA UKWELI NDANI YA MOYO WANGU, NIPO TAYARI KUJIREKEBISHA NA KUWA WAKO
DAIMA. AMINA.
No hay comentarios:
Publicar un comentario