JUMAPILI
YA 14 YA MWAKA-B
12/7/2015
Somo
I: Amo: 7:12-15
Zab:
84:9-14
Somo
II: Efe 1:3-14
Injili:
Mk 6:7-13
Nukuu:
“Ndipo Amosi akajibu akamwambia Amazia, Mimi sikuwa nabii,
wala sikuwa mwana wa nabii; bali nalikuwa mchungaji, na mtunza mikuyu; naye Bwana akanitwaa, katika kufuatana
na kundi; Bwana akaniambia, Enenda uwatabirie watu wangu Israeli,” Amo 7:14-15
“Kwa kuwa alitangulia kutuchagua, ili tufanywe wanawe kwa njia ya
Yesu Kristo, sawasawa na uradhi wa mapenzi yake,” Efe 1:5
“Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha
ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake,” Efe 1:7
“Naam, katika
yeye huyo; na ndani yake sisi nasi tulifanywa urithi, huku tukichaguliwa tangu
awali sawasawa na kusudi lake yeye, ambaye hufanya mambo yote kwa shauri la
mapenzi yake,” Efe 1:10b-11
“Nanyi pia katika huyo mmekwisha kulisikia neno la kweli, habari
njema za wokovu wenu; tena mmekwisha kumwamini yeye, na kutiwa muhuri na Roho
yule wa ahadi aliye,” Efe 1:13
“akawakataza
wasichukue kitu cha njiani isipokuwa fimbo tu; wala mkate, wala mkoba, wala
pesa za bindoni; lakini wajifungie
viatu; akasema, Msivae kanzu mbili,” Mt 10:8-9
“Akawaambia, Mahali po
pote mtakapoingia katika nyumba, kaeni humo hata mtakapotoka mahali pale,” Mt
10:10
“Na mahali po pote
wasipowakaribisha ninyi wala kuwasikia, mtokapo huko, yakung'uteni mavumbi
yaliyo chini ya miguu yenu, kuwa ushuhuda kwao,” Mt 10:11
TAFAKARI:
“Hatupo kwa ajili yetu wenyewe, yote ni kwa neema ya Mungu.”
Wapendwa wana wa Mungu,
kile ulicho na yale yote uyafanyayo si
kwa ajili yako mwenyewe, bali yamekuwa kama yalivyo kwa neema Mungu. Hakika
hatuna kitu chochote tunachoweza kujivunia kama mali yetu binafsi. Vyote
tumepewa kwa muda tu, na kama uangalizi. Ndugu yangu, fursa uliyonayo leo si
bahati mbaya, ila kwa kupitia wewe Mungu ajulikane kwa wengine. Tunapotambua
ukweli huu Mungu kamwe hatoacha kututumia kama apendavyo. Hivyo Nabii Amosi
anatambua ukweli huu na kusema, “Mimi
sikuwa nabii, wala sikuwa mwana wa nabii; bali nalikuwa mchungaji, na mtunza
mikuyu; naye Bwana akanitwaa,
katika kufuatana na kundi; Bwana akaniambia, Enenda uwatabirie watu wangu
Israeli,” Amo 7:14-15. Ukweli huu pia
utunyenyekeza.
Wapendwa
wana wa Mungu, yale yote tufanikiwayo na yenye mwono wa Mungu, ni uchanguzi
wake Mungu mwenyewe na wenye mwelekeo wa ukombozi pale ulipo na umilele kwa
kile ukitarajiacho. “Kwa kuwa alitangulia kutuchagua, ili tufanywe wanawe kwa njia ya
Yesu Kristo, sawasawa na uradhi wa mapenzi yake,” Efe 1:5. Je, najitambua
napoyaona mafanikio yangu kuwa ni mkono wa Mungu anayetaka kuyafanya hayo kwa
wale wanaonizunguka kupitia Yeye Mwenyewe? Ukombozi wetu bila Kristo ni ndoto
isiyowezekana. Hakuna yeyote awezaye kutukomboa isipokuwa Yesu mwenyewe. “Katika yeye huyo, kwa damu
yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema
yake,” Efe 1:7. Ni kupitia Kristo tunapata masamaha wa dhambi zetu na kuwa huru
kutoka utumwa wa dhambi zetu.
Wapendwa
wana wa Mungu, leo hii tu warithi wa ufalme wa Mungu kwa sababu tumekombolewa
kwa damu ya Kristo. “Naam, katika yeye huyo; na ndani yake sisi nasi tulifanywa
urithi, huku tukichaguliwa tangu awali sawasawa na kusudi lake yeye, ambaye
hufanya mambo yote kwa shauri la mapenzi yake,” Efe 1:10b-11. Kwa warithi wa
ufalme wa Mungu ni kuwa na uhakika wa kuishi milele. Jambo hili kwa upande
mwingine haliwezi kutokea kama hatutatimiza wajibu wake. Kila mmoja wetu kwa ukiri
wake mbele ya Kristo yampasa kuishi kadiri ya ahadi zetu za ubatizo.
Kwa
ukombozi tulioupata kupitia Kristo sisi sote tumepewa muhuri wa Roho Mtakatifu.
Ukweli ndiyo utakao tuweka huru na kweli hiyo ndiyo kielelezo cha yale yote
tuyafanyayo. “Nanyi pia katika huyo mmekwisha kulisikia neno la kweli, habari
njema za wokovu wenu; tena mmekwisha kumwamini yeye, na kutiwa muhuri na Roho
yule wa ahadi aliye,” Efe 1:13. Tupo huru ndani na katika Kristo. Imani yetu
bila Kristo ni sawa na kurusha ngumi kwenye upepo.
Tunapoyaishi
haya katika uhasilia wake, maisha hayo yote yanatulazimu kufanya kinyume cha
yale tuliyoyazoea. Yesu “akawakataza wasichukue kitu cha njiani isipokuwa fimbo tu; wala
mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni; lakini wajifungie viatu; akasema, Msivae kanzu mbili,” Mt
10:8-9. Fimbo ni ishara ya mamlaka ambayo kwayo tumepewa na siyo kujitwalia
wenyewe. Mamlaka haya si katika nguvu na kutawala, ila nguvu zitokanazo na
maadili mema. Na katika kutenda kwetu, yatupasa kufanya jambo moja kwa wakati
na siyo kujichanganya kwa mambo mengi kwa wakati mmoja. Yesu “Akawaambia, Mahali po pote mtakapoingia katika nyumba, kaeni
humo hata mtakapotoka mahali pale,” Mt 10:10. Katika utume wetu, yatupasa
kufanya kile tulichokusudia kukifanya bila kujibakiza. Tulifanyalo jambo hilo
kwa uaminifu mambo hayawezi kwenda sawa kila wakati. Tutegemee upinzani wakati
mwingine na hata kukataliwa. “Na mahali po pote
wasipowakaribisha ninyi wala kuwasikia, mtokapo huko, yakung'uteni mavumbi
yaliyo chini ya miguu yenu, kuwa ushuhuda kwao,” Mt 10:11. Tendo hili la kukung’uta mavumbi ya miguu la
maanisha kwamba waliotufukuza au kutokupokea yale tuliyowaambia yaliyo kweli,
ni kweli hiyo hiyo itakayowahukumu.
Ndugu yangu, tupo kwa
ajili ya wengine na kile tulicho si kwa sababu yetu wenyewe.
Tumsifu Yesu Kristo!
No hay comentarios:
Publicar un comentario