IJUMAA
WIKI YA 6 YA PASAKA-B
15/5/2015
Somo:
Mdo 18:9-18
Zab:
46
Injili:
Yoh 16:20-23a
Nukuu:
“Hata
Galio alipokuwa liwali wa Akaya, Wayahudi wakamwinukia Paulo kwa nia moja,
wakamleta mbele ya kiti cha hukumu, wakisema
Mtu huyu huwavuta watu ili wamwabudu Mungu kinyume cha sharia,” Mdo 18:12-13
“bali
ikiwa ni hoja juu ya maneno na majina na sheria yenu, liangalieni ninyi
wenyewe, maana mimi sitaki kuwa mwamuzi wa mambo hayo,” Mdo 18:15
“Amin,
amin, nawaambia, Ninyi mtalia na kuomboleza, bali ulimwengu utafurahi; ninyi
mtahuzunishwa, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha,” Yoh 16:20
“Basi
ninyi hivi sasa mna huzuni; lakini mimi nitawaona tena; na mioyo yenu
itafurahi, na furaha yenu hakuna awaondoleaye,” Yoh 16:22
TAFAKARI:
“Furaha katika Mateso”
Wapendwa wana wa Mungu,
leo tutafakari neno hili kadiri ya masomo yetu ya leo, “Furaha katika Mateso.”
Licha ya kuwa na mitazamo tofauti kuhusu mateso kadiri ya Imani zetu, uhalisia
wa mateso ni mang’amuzi ambayo kila mmoja wetu anaweza kuuelezea. Wapo ambao
wameenda mbali zaidi na kusema kwamba kitendo cha mtoto mdogo kulia baada ya
kuzaliwa tu, ni ujumbe kwetu kwamba dunia hii tunayoishi hatuwezi kuitenganisha
na mahangaiko na mateso yetu.
Mateso
ni hali na ni sehemu ya maisha ya binadamu yeyote bila kujali imani yake. Ila
"mateso" huwa na maana tu katika sababu na tafsiri yake.
Swali:
-Nini
sababu ya mateso yangu?
-Nini
sababu ya uwepo wetu?
-je,
kuna maana yeyote ya mimi kuwepo?
-kama
ipo malengo yake nini hasa kwa hali hii niliyonayo sasa?
Wapendwa
yapo majibu rahisi hasa pale tu tunapojua chanzo chake.
Mfano;
1.
kuna magonjwa ambayo tunayapata tukijua chanza chake ni nini, tiba yake, na
matokeo yake hujulikana. Hapa mwathirika ni kufuata ushauri wa daktari yote
huueleweka.
2.
Yapo pia mateso kutokana na magonjwa fulani twajua tu chanzo chake, ila tiba na
kupona kwake bado ni kitendawili kikubwa.
3.
Yapo pia mateso ambayo uelekea kuwa na magonjwa ambayo hatujui chanzo chake,
tiba yake, na mwisho hatujui kupona kwake. Hapa binadamu hupita katika uvuli
mzito wa umauti. Hapa pia yawezekana kukawa na Mateso tu ambayo si ugonjwa ila
ni hali ya "sintofahamu." Unakuta unateseka ila huna maelezo
yanajitosheleza.
Aina
hii ya tatu ina ugumu sana kwa binadamu kuipokea. Tunajisikia kutengwa hata
kutokuona umaana wa Mungu kwetu kama (upendo wake, uwezo wake na hata umuhimu
wake)
Bila
tafsiri yenye kujumuisha, "sababu, lengo, na uwepo wa Yesu katika historia
nzima ya wokovu wetu," ni vigumu kuona maana, lengo, na FURAHA katika
mateso yetu kwa ujumla
na
zaidi kwa kipengele cha tatu.
Ni
ndani ya Yesu Kristo, na katika Yesu Kristo twaweza elewa "fumbo" la
TESO na siyo "jibu" lake. Ufahamu huu ukiwepo basi ni mwanzo wa
FURAHA katika TESO lolote lile.
Jambo la kufahamu:
Teso
au mateso si jambo au hali ya kudumu milele likiwa ndani ya Yesu Kristo na
katika Yesu Kristo. Rejea;
-Mt 4:24,
-Mt 16:21
-Mk 8:31,
-Lk 9:22,
-Lk
16:28, -Lk 17:25,
-Lk
24:26,
-Rom 8:18
2 Kor
1:6, 2 Kor 1:7
-Wafp
3:10, -Wakol 1:24
2 Tim
1:12, 2 Tim 3:11
1 Pet
4:13, 1 Pet 5:9
Ufu 1:9
Kwa
kushiriki ubinadamu wetu na katika safari ya wokovu wetu, Yesu Kristo kaondoa
umilele wa Teso/mateso yetu na kulipa/kuyapa maana. Akiwa ndiye Njia, ukweli,
na uzima (Yoh 14:6), Yesu anachagua njia ya mateso kutupatia wokovu wetu. Hapa
ndipo mateso au teso huwa na maana ndani ya Yesu Kristo na kwa ajili ya Yesu
Kristo.Twashiriki pia mateso na wengine katika Kristo tukitambua ukweli huo wa
fumbo la teso kwa njia ya sala na majitoleo yetu tukiwa katika muunganiko na
Kristo.
Wapendwa
wana wa Mungu, Mtume Paulo anaburuzwa na Wayahudi mbele ya Mahakama ya Kirumi
kushtakiwa kwa kosa la kuwavuta watu ili wamwabudu Mungu. Je, kunakosa lolote
kumwabudu Mungu? Kumwabudu Mungu kama tendo la kujisalimisha kwake ndiyo njia
pekee ya kujenga mahusiano yetu na Mungu ya karibu. Ndio njia pekee ya kuzijua siri
na ufahamu wa Kimungu. Kwa Mtume Paulo mambo yalikuwa kama hivi: ““Hata Galio alipokuwa
liwali wa Akaya, Wayahudi wakamwinukia Paulo kwa nia moja, wakamleta mbele ya
kiti cha hukumu, wakisema Mtu
huyu huwavuta watu ili wamwabudu Mungu kinyume cha sharia,” Mdo 18:12-13. Kwa
vile Mtume Paulo alisimama katika kweli na haki, Galio anawashangaa Wayahudi
kwa madai yao juu ya Paulo, naye anasema, “bali
ikiwa ni hoja juu ya maneno na majina na sheria yenu, liangalieni ninyi
wenyewe, maana mimi sitaki kuwa mwamuzi wa mambo hayo,” Mdo 18:15. Tukio hili
ni mateso katika furaha. Ni furaha kwa sababu tunajua tunateseka katika kweli,
ila hatujui kwa nini tunateswa, na watesi wetu wameingiwa upofu wa kujui kweli.
Mtume Paulo analitambua jambo hili kwa undani kabisa na hivyo anasema, “kwa
maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu kama utukufu ule
utakaofunuliwa kwetu,” Rum 8:18
Kuyaona mateso katika
mtazamo huu wa Mtume Paulo ni kukomaa katika Imani, na kujua kusudi la malengo
yako hapa duniani. Malengo yetu hapa duniani ni ya muda mfupi, ukilinganisha na
umilele baada ya maisha haya. Yesu Kristo anatufumbulia jambo hili katika
injili ya leo kwa kusema, “Amin, amin,
nawaambia, Ninyi mtalia na kuomboleza, bali ulimwengu utafurahi; ninyi
mtahuzunishwa, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha,” Yoh 16:20. Wito wa
Bwana wetu Yesu Kristo kuhusu mateso ni kwamba yatupasa kutazama mbele zaidi
yaani kile kitakacho kuwa baada ya mateso hayo. Kwa hiyo ni lazima kuona na
kutambua kiini cha mateso yetu, na mahusiano yake ndani na katika Kristo.
Wapendwa wana wa Mungu,
furaha halisi na isiyo na kikomo ni furaha ya kuteseka pamoja na Kristo na
kufufuka pamoja naye. Kuteseka pamoja na Kristo ni kuyatazama mateso yote ndani
na katika Kristo, na kumshirikisha mateso hayo ambayo kwayo yeshapewa maana na
Kristo. Maana ya mateso katika Kristo ni USHINDI. Kristo kayashinda mateso na
kwake tu, mateso huwa maana. Hivyo, “Basi
ninyi hivi sasa mna huzuni; lakini mimi nitawaona tena; na mioyo yenu
itafurahi, na furaha yenu hakuna awaondoleaye,” Yoh 16:22. Furaha hii baada ya
ushindi huu wa mateso ndani na katika Kristo, ni furaha ya kweli na isiyo na
kikomo.
Ndugu yangu tusisahau
maneno haya mazito ya Bwana wetu Yesu Kristo; “Kwani atafaidiwa nini mtu
akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini
badala ya nafsi yake?” Mt 16:26. Kuyakimbia mateso ndani na katika Kristo ni
kuukimbia utukufu wa Mungu.
Tumsifu Yesu Kristo!
BWANA WETU YESU KRISTO TUPE UWEZO WA KUYAPOKEA YOTE
KATIKA WEWE NA NDANI YA WEWE ILI TUPATE MAANA NA FURAHA KATIKA MATESO YETU NA
YA WENZETU. AMINA
No hay comentarios:
Publicar un comentario