JUMAMOSI WIKI YA 22 YA MWAKA-I
Somo: Kol 1:21-23
Zab: 54:2-3, 5 na 7.
1
Ee Mungu,
uyasikie maombi yangu, Uyasikilize maneno ya kinywa changu. Kwa maana wageni
wamenishambulia; Watu watishao wananitafuta nafsi yangu; Hawakumweka Mungu
mbele yao.
(K) Bwana ndiye
msaada wangu
2 Atawarudishia adui zangu ubaya wao; Uwaangamize
kwa uaminifu wako. Kwa kuwa limeniokoa na kila taabu; Na jicho langu
limeridhika Kwa kuwatazama adui zangu. (K)
Injili: Lk 6:1-5
Nukuu:
“Na ninyi, mliokuwa hapo
kwanza mmefarikishwa, tena adui katika nia zenu, kwa matendo yenu mabaya,
amewapatanisha sasa; katika mwili wa nyama yake, kwa kufa kwake,” Kol 1:21-22a.
“Akawaambia, Mwana wa
Adamu ndiye Bwana wa sabato,” Lk 6:5.
TAFAKARI: “Kristo katuweka huru, hivyo tusimame katika kweli kila siku.”
Wapendwa wana Mungu, Kristo katuweka huru, hivyo tusimame
katika kweli kila siku. Kusimama katika kweli ni kuthamini na kuishi kweli ya
Mungu na kuwa na hofu yake. Hofu ya Mungu tuliyonayo msingi wake ni upendo wa
Mungu hasa kwa kumtoa mwanaye mpenzi kama sadaka, na kututoa kutoka utumwa wa
dhambi. Ukombozi wetu ni wa gharama kubwa sana. Je, wauthamini Ukristo wako kwa
kuishi Imani ya kweli? Mtume Paulo anatukumbusha habari hii kwa kusema, “Na ninyi, mliokuwa hapo kwanza mmefarikishwa, tena adui katika
nia zenu, kwa matendo yenu mabaya, amewapatanisha sasa; katika mwili wa nyama
yake, kwa kufa kwake,” Kol 1:21-22a.
Ni kwa
mantiki hiyo hapo juu kwamba Kristo ndiye kielelezo cha yote yale tuyafanyayo
ili tuurithi ufalme wa Mbingini tulioandaliwa na kuutamani. Je, yale yote
niyafanyayo leo na sasa yanaendana na sadaka ya Yesu pale msalabani? Yesu
anataka Wayahudi, na wewe na mimi tuelewe kwamba yale tuyafanyayo yaendane na
thamani ya upendo wa Mungu kwetu, na Yeye, yaani Kristo ndiye msingi wa vyote. Kristo
akiwa msingi wa maisha yetu na sababu ya yale yote tuyafanyayo, basi tutakuwa
huru kweli kweli kwa sababu tutajua ni nini tunayemtumikia. Hivyo Yesu
anawaambia Wayahudi “Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato,” Lk 6:5. Kristo
ndiye mizania ya kweli kuhusu Mungu tunayemwamini na kumwabudu. Kristo ndiye
anayejua siri ya ufalme wa Mungu, na kwa kupitia Yeye nasi tunafunuliwa siri
hiyo. Ndugu yangu Kristo ndiye njia, kweli na uzima, Yoh 14:6.
Tumsifu
Yesu Kristo!
“Akawaambia, Mwana wa Adamu ndiye
Bwana wa sabato,” Lk 6:5.
Tusali:-Ee Yesu kwako tu
huru.
No hay comentarios:
Publicar un comentario