IJUMAA WIKI YA 22 YA MWAKA-I
Somo: Kol 1:15-20
Zab: 100: 1b-2, 3, 4,5
1 Dunia yote; Mtumikieni Bwana kwa furaha; Njoni mbele zake kwa
kuimba.
(K) Njoni mbele
zake Bwana kwa kuimba.
2 Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu; Ndiye aliyetuumba na sisi tu
watu wake; Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. (K)
3 Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; Nyuani mwake kwa
kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake. (K)
4
Kwa kuwa Bwana
ndiye mwema; Rehema zake ni za milele; Na uaminifu wake vizazi na vizazi. (K)
Injili: Lk 5:33-39
“Kwa kuwa katika yeye vitu
vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na
visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu
vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake,” Kol 1:16.
“Lakini Yesu akawaambia, Je! Mwaweza kuwafanya
wafunge walioalikwa arusini, akiwapo bwana arusi pamoja nao?” Lk 5:34.
“Lakini divai mpya sharti kutiwa katika viriba vipya,” Lk
5:38.
“Wala
hakuna anywaye divai ya kale akatamani divai mpya; kwa kuwa asema, Ile ya kale
ndiyo iliyo njema,” Lk 5:39.
TAFAKARI: “Nguvu na mamlaka ya Kristo ni uthibitisho wa ujemedari
wake dhidi ya uovu.”
Wapendwa wana wa Mungu, mamlaka aliyokuwa nayo Yesu ni vita
na ushindi dhidi ya uovu hapa duniani. Ni ukweli usiopingika kwa kupitia jina
lake tunapata uponyaji wa kweli, Mdo 4:12. “Lakini
Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho
nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende,” Mdo 3:6. “Mamlaka ya Yesu yamejengwa chini ya mamlaka ya
Mungu. Hivyo hakuna jambo lolote alifanyalo Yesu Lisilo kuwa na uhusiano na
Mungu, huku jambo lile likifunua siri ya Mungu kila kukichwa. “Kwa kuwa
katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi,
vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi,
au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake,” Kol 1:16.
Kwa nini basi nakuwa na mashaka juu ya utendaji wa Kristo katika maisha yangu?
Wapendwa
katika Kristo, Yesu anapotoa mfano wa vazi kuukuu na jipya, na kwa upande
mwingine divai ya zamani na kiriba cha kipya anataka kutufundisha jambo hili; kwanza
kabisa lazima tujue sababu na malengo ya maisha yetu hapa tuniani. Hatupo hapa
duniani kwa bahati mbaya hata kidogo. Tupo katika ulimwengu huu kadiri ya mpango
wa Mungu ambao ni dhahiri na mathubuti. Hivyo lolote lile lililo jema mbele ya
Mungu huwiishwa na kufanya upya. Katika Injili ya leo tunaona watu wakimletea
Yesu malalamiko juu ya kufunga na kuomba. Kufunga kwetu na kuomba kwetu
uifaidia kwanza kabisa roho zetu na wenzetu. Tunawajibu huo kiimani, na
yatupasa kuutekeleza pasipo imani na msaada wowote. Ndiyo maana Yesu anawauliza
watesi wake swali hili: “Je! Mwaweza kuwafanya
wafunge walioalikwa arusini, akiwapo bwana arusi pamoja nao?” Lk 5:34. Maisha yapaswa
kusherehekewa kwa sababu ni mali na zawadi ya Mungu.
Hivyo basi, upya wetu kiimani hutoshelezwa na upya
tuupokeao kwa Yesu tunaposhiriki sakramenti zake tukiwa katika hali ya usafi.
Hivyo “divai mpya sharti kutiwa katika viriba vipya,” Lk 5:38. Ndani na katika
Kristo kiimani hujengeka kwa matendo madogo madogo yanayompendeza Mungu. “Wala
hakuna anywaye divai ya kale akatamani divai mpya; kwa kuwa asema, Ile ya kale
ndiyo iliyo njema,” Lk 5:39. Ndugu yangu ukiona vinaelea ujue vimeundwa.
Tumsifu Yesu Kristo!
“Lakini
divai mpya sharti kutiwa katika viriba vipya,” Lk 5:38.
Tusali:-Ee Yesu Mwema, tuimarishe katika imani, na tuishi katika
kweli yako. Amina
No hay comentarios:
Publicar un comentario